Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

SERIKALI imesema kumekuwa na ongezeko kubwa la magonjwa yasiyoambukiza kwa kipindi cha miaka ya hivi karibuni hali inayotishia afya ya mama na mtoto wakati wa kijifungua pindi wanapofika hospitalini.

Hayo yamesemwa leo jijini Dar es Salaam na Kaimu Mkurugenzi wa Magonjwa yasiyokuwa ya kuambukiza kutoka Wizara ya Afya,Maedeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dk . Sara Maongezi wakati akifungua Programu ya AstraZeneca ya Healthy Heart Africa (HHA).

Programu hiyo inatokana na ushirikiano wa Touch Foundation na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.Lengo ni  kupunguza maradhi ya shinikizo la damu wakati wa mimba.

Maongezi amefafanua ubia uliozinduliwa leo katika mradi huo utakaoongeza utekelezaji wa programu hiyo nchini Tanzania.  

"Ubia huo unakusudia kwa kiasi kikubwa kupunguza kuenea kwa maradhi ya shinikizo la damu, hasa miongoni mwa wanawake wajawazito ikiwa ni kuunga mkono mpango mkakati wa Serikali wa kuzuia na kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza,"amesema Dk. Maongezi.

Ameongeza kupanda kwa shinikizo la damu ni moja ya vihatarishi vikubwa vya ugonjwa wa moyo hali ambayo msukumo wa damu katika moyo  huzuizwa au kukatizwa na chembe chembe za mafuta kwenye mishipa ya koronari  na mwishowe huenda ikasababisha kiharusi.

Amefafanua kwa bahati mbaya, ugonjwa wa moyo ni moja ya vyanzo vikubwa vya kifo nchini Tanzania hasa kwa wajawazito wakati wa kujifungua.

Amesema  kupitia ufadhili wa AstraZeneca, shirika la Touch Foundation litaendeleza mpango wa Healthy Heart Africa  ambao tayari unatekelezwa huko Kenya na Ethiopia, kwa kufuata mazingira halisi ya Tanzania kama linavyotekelezwa mpango wake wa Mobilizing Maternal Health (MMH) katika mikoa ya Shinyanga na Mwanza.

 "Serikali tunaukaribisha ubia huu mpya kwa vile unakwenda sambamba na azma yetu inayolenga kinga kwa jamii, kuboresha afya, kupima, na kutoa matibabu mapema, na kuwasaidia waathirika. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...