Fursa ya kwanza ya uandaaji wa mashindano maarufu ya mbio za mbuzi imekua ya mafanikio kwa Klabu ya Rotary ya Oysterbay. Tukio hilo lenye burudani ya aina yake lilikwenda kwa Motto wa ‘Wakanda Goat are You’, na kuvuatia watu zaidi ya 4,500 waliokusanyika katika eneo la The Green, Oysterbay kwa ajili ya kushuhudia mashindano hayo. 

Matukio muhimu yaliyofuata baada ya mbio hizo ni mchezo wa bahati nasibu ambao uliwezeshwa na wafadhili wa hapa nyumbani pamoja na gwaride la kuonyesha mavazi, ambapo watu mbalimbali walipata fursa ya kuonyesha mavazi yao aina ya Wakanda kwa kurejelea mafanikio ambayo muvi ya Marvel ya ‘Black Panther’ imeyapata kwa mwaka huu.

Ni mwaka wa kumi na nane mfululizo wa mashindano hayo lakini kwa mwaka wa kwanza chini ya Rotary Goat Races, tukio hili maarufu la kifamilia lilivutia maelfu ya watu siku ya tarehe 23 Juni. Tukio hilo likifanyika katika eneo la ‘The Green’ chini ya motto wa ‘Wakanda Goat are You”, wahudhuriaji walifurahia aina saba za mbio, vyakula vya aina mbalimbali vya hapa nyumbani, zawadi kubwa mbalimbali za bahati nasibu, michezo ya kuweka dau na gwaride la ushindani la mavazi ya Wakanda.

Mashindano hayo yalianza kwa mbuzi kusimama kwenye mstari wa mwanzo wa mashindano, huku watazamaji wakivuta pumzi kuona mbuzi wanavyopigania ushindi wa kuwa namba moja.

KAtika raundi ya kwanza Mbuzi aliyeibuka kidedea ni namba 8 ambapo zawadi yake ilidhaminiwa na Kampuni ya vinywaji ya CocaCola, Raundi ya pili mbuzi namba 7 aliibuka mshindi na zawadi yake kudhaminiwa na East Africa TV/Radio huku raundi ya tatu mbuzi namba tisa akikiibuka mshindi na zawadi yake kudhaminiwa na Kampuni ya Aggreko. 
Washiriki wa mashindano ya mbio za mbuzi wakiwa wamewabeba mbuzi wao tayari kushiriki mbio hizo wakati wa hafla ya mashindano hayo maarafu ambayo yaliyofanyika katika eneo la The Green, Oysterbay jijini Dar es Salaam wikiendi hii. Kwa mwaka huu mashindano hayo ya kufana yaliandaliwa na Klabu ya Rotary Dar es salaam, Oysterbay ambapo yalivutia zaidi ya watu 4,500 huku yakiwa chini ya Motto wa ‘Wakanda Goat Are You’? yakirejerelea mafanikio ambayo muvi ya Marvel ya ‘Black Panther’ imeyapata kwa mwaka huu.
Washiriki wa mashindano ya mbio za mbuzi wakiwakimbiza mbuzi wao wakati wa hafla ya mashindano hayo maarafu ambayo yaliyofanyika katika eneo la The Green, Oysterbay jijini Dar es Salaam wikiendi hii. Kwa mwaka huu mashindano hayo ya kufana yaliandaliwa na Klabu ya Rotary Dar es salaam, Oysterbay ambapo yalivutia zaidi ya watu 4,500 huku yakiwa chini ya Motto wa ‘Wakanda Goat Are You’? yakirejerelea mafanikio ambayo muvi ya Marvel ya ‘Black Panther’ imeyapata kwa mwaka huu.
Anne Saels, Rais wa Klabu ya Rotary Dar es salaam, Oysterbay akizungumza na waandishi wa habari wakati wa hafla ya mashindano ya mbio za mbuzi yaliyofanyika katika eneo la The Green, Oysterbay jijini Dar es Salaam wikiendi hii. Kwa mwaka huu mashindano hayo ya kufana yaliandaliwa na Klabu ya Rotary Dar es salaam, Oysterbay ambapo yalivutia zaidi ya watu 4,500 huku yakiwa chini ya Motto wa ‘Wakanda Goat Are You’? yakirejerelea mafanikio ambayo muvi ya Marvel ya ‘Black Panther’ imeyapata kwa mwaka huu.
Anne Saels, Rais wa Klabu ya Rotary Dar es salaam, Oysterbay akizungumza na waandishi wa habari wakati wa hafla ya mashindano ya mbio za mbuzi yaliyofanyika katika eneo la The Green, Oysterbay jijini Dar es Salaam wikiendi hii. Kwa mwaka huu mashindano hayo ya kufana yaliandaliwa na Klabu ya Rotary Dar es salaam, Oysterbay ambapo yalivutia zaidi ya watu 4,500 huku yakiwa chini ya Motto wa ‘Wakanda Goat Are You’? yakirejerelea mafanikio ambayo muvi ya Marvel ya ‘Black Panther’ imeyapata kwa mwaka huu. 
Anne Saels, Rais wa Klabu ya Rotary Dar es salaam, Oysterbay akizungumza na waandishi wa habari wakati wa hafla ya mashindano ya mbio za mbuzi yaliyofanyika katika eneo la The Green, Oysterbay jijini Dar es Salaam wikiendi hii. Kwa mwaka huu mashindano hayo ya kufana yaliandaliwa na Klabu ya Rotary Dar es salaam, Oysterbay ambapo yalivutia zaidi ya watu 4,500 huku yakiwa chini ya Motto wa ‘Wakanda Goat Are You’? yakirejerelea mafanikio ambayo muvi ya Marvel ya ‘Black Panther’ imeyapata kwa mwaka huu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...