Na. Andrew Chimesela, Morogoro

Mafunzo ya kubaini mahitaji ya watumishi kwa kutumia mfumo unaojulikana kwa jina la kitaalamu Workload Indicators of Staffing Needs - WISN na Prioritaization and Optimization analysis – POA (WISN plus POA)  yaliyoanza Juni 4 mwaka huu katika ukumbi wa ICE wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoinne – SUA Mkoani Morogoro yamehitimishwa Juni 8 kwa mafanikio makubwa.
Akiongea na washiriki wenzake wakati wa Kufunga mafunzo hayo Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Utawala na Rasilimali Watu  Mkoa wa Kilimanjaro Bw. Sebastian Masanja amewapongeza wakufunzi wa mafunzo hayo kwa kujitahidi kuwapa kile walicholenga kutoa hadi wao kuelewa  kwa ufanisi na kwa niaba ya wenzake ameahidi kwenda kuyafanyia kazi mafunzo hayo katika Halmashauri zao.
Bw. Masanja ambaye alikuwa mgeni rasimi katika kufunga mafunzo hayo amewataka washiriki wenzake kutambua kuwa hadi sasa watumishi wa Serikali hususan wa kada ya Afya bado hawatoshelezi kwenye vituo vya kutolea huduma, hivyo ni wajibu wao kutumia mafunzo waliyoyapata kuisaidia Serikali kuwapanga vizuri watumishi waliopo kulingana na uzinto wa kazi.
“Washiriki wenzangu, tumeshajifunza kuwa kituo cha Afya kilichopo Mjini hakiwezi kulingana majukumu yake na uzito wake wa kazi na kituo cha Afya cha kijijini, kwa sababu hata idadi ya wagonjwa inatofautiana, kwa hiyo tuisaidie Serikali kuondoa malalamiko  kwa kuwapanga vizuri watumishi waliopo kulingana na uzito wa kazi zinazopatikana kwenye maeneo husika” alisema Bw. Masanja.
Baadhi ya timu ya  viongoi wa mafunzo ya WISN PLUS POA wakiwa tayari kukabidhi vitabu vilivyoandaliwa kwa ajili ya kutekeleza kile walichojifunza washiriki wa mafunzo hayo. Kutoka kushoto ni Gracian Makota, Renatus Mashauri na Bw. Sebastian Masanja. Wengine ni wenyekiti wa washiriki wakati wa mafunzo na David Laput Mratibu wa PS 3 Mkoa wa Morogoro.
Bw. Sebastian Masanja ambaye pia ni Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Utawala, Mkoa wa Kilimanjaro aliyefunga mafunzo hayo akimkabidhi vitabu Mmoja wa washiriki wa mafunzo ya WISN PLUS POA SUA Mkoani Morogoro.  DSCN1936
Mgeni Ramsi aliyefungua mafunzo ya WISN PLUS POA Dkt. Frank Jacob (katikati waliokaa) ambaye pia ni Mganga Mkuu wa Mkoa wa Morogoro akiwa katika picha ya pamoja na washiriki wa mafunzo hayo kutoka Mikoa ya Morogoro na Dodoma yaliyofanyika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine. Kwa habari kamili BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...