*Uchache wa mabasi wasababisha mlundikano wa abiria vituoni

Humphrey Shao, Globu ya Jamii
MBUNGE wa Ubungo jijini Dar es Salaam Saed Kubenea ameishauri Serikali kuifuta kodi kwa mabasi ya mwendokasi 70 yanayotarajiwa kuingia nchini kwa lengo la kurahisisha usafiri katika mradi huo ambao kwa sasa unasua kutokana na kuzidiwa na wingi wa abiria.

Kubenea ametoa ushauri huo leo baada ya kutembelea Kituo cha mabasi ya Mwendokasi cha Kimara Mwisho ili kuangalia changamoto zilizopo katika mradi wa mabasi yaendayo Haraka (Udart).

Akiwa katika kituo hicho Kubenea ameambiwa changamoto kubwa iliyopo ni uhaba wa wa mabasi hayo ukilinganisha na wingi wa abiria wanaotumia usafiri huo.

"Niishauri Serikali ifute kodi ili haya mabasi yaweze kuingia au itoe muda fulani wa kulipa kodi angalau miezi sita hivi huku usafiri ukiendelea kutumika.

"Inawezekana mabasi hayo yanashindwa kuingia kwasababu mhusika amekosa kodi ya kulipa ndio maana yanachelewa na matokeo yake kusababisha adha ya usafiri kwa abiria kurundikana kwenye vituo kutokana na uhaba wa mabasi hayo,"amesema Kubenea.

Kubenea amesema wao kama wabunge wa Dar es Salaam pamoja na madiwani watahakikisha wanaulinda mradi huo ili udumu kwa ajili ya kizazi kijacho.

"Dar es Salaam ni kitovu cha nchi kibiashara, hivyo usafiri unapokuwa wa shida unaathiri mambo mengine. Sisi kama wabunge tunaowajibu wa kuulinda mradi huu na tutahakikisha tunaulinda,".

Ameongeza atazungumza na wabunge pamoja na Waziri wa Tamisemi kujua wanafanyaje kuulinda mradi huo pamoja na kupata eneo kwa ajili ya karakana.

Aidha Kubenea amesema mfumo mpya wa kielektroniki wa malipo serikalini (GePG) ni mzuri na utasaidia katika kuokoa wanaokwepa kodi na upotevu wa fedha.

Mbunge wa Ubungo, Saed Kubenea akizungumza na Maofisa wa kitengo cha habari cha mradi wa mabasi yaendayo kasi (UDART) mara baad ya kutembelea mradi wa huo na kujionea mapungufu yaliyojitokeza na kusisitiza kuwa kila mbia ahakikishe changamoto zilizopo zinamalizika haraka.
 Mbunge wa Ubungo Saed Kubenea akimsikiliza mmoja wa Watendaji wa kitengo cha habari katika mradi wa UDART , Joel Beda wakati alipofika  makao makuu ya ofisi hizo Jangwani jijini Dar es Salaam.
Mbunge wa Ubungo Saed Kubenea akiwa ndani ya moja ya mabasi yaendayo kasi mara kuchanganyika na wananchi.
Mbunge wa Ubungo Saed Kubenea akisikiliza maelekezo kutoka kwa mmoja ya watendaji wa UDART Katika kituo cha Kimara ambapo alikwenda kujionea msongamano wa abiria katika eneo hilo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...