Na Mwandishi wetu
MJUMBE maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa nchi za Maziwa Makuu (ICGLR), Said Djinnit ametaka nchi wanachama wa Umoja wa Ushirikiano katika masuala ya kisheria katika nchi hizo za ICGLR , kuongeza kasi ya mashirikiano ili kukabiliana na uhalifu dhidi ya ubinadamu.
Nchi zinazounda umoja wa ICGRL pamoja mwenyeji Tanzania ni Angola, Burundi, Jamhuri ya Afrika ya kati, Congo, Kenya, Rwanda, Sudan, South Sudan, Uganda na Zambia.
Alisema pamoja na kufikia maendeleo ya kutosha katika ushirikiano wa kisheria nchi hizo kwa sasa zinatakiwa kuungana zaidi kutokana na watenda uhalifu dhidi ya ubinadamu kuendelea kujificha katika nchi mbalimbali.
Akizungumza katika mkutano wa pili wa umoja huo uliofanyika jijini Dar es salaam jana, Djinnit alisema kwamba mambo makubwa mazuri yamefanyika miongoni mwa nchi hizo tangu kuuanzishwa kwa ushirikiano huo, na kutaka wazidi kujiimarishwa sanjari na ushirikiano mwingine wa kukomesha uhalifu.
Alisema bila kukomeshwa kwa uhalifu dhidi ya ubinadamu mataifa ya Maziwa makuu yatakuwa katika hekaheka na hiyvo kukosa maendeleo kutokana na kukosekana kwa amani.
Awali akmimkaribisha mjumbe huyo kufungua mkutano, Naibu Mkurugenzi Mwendesha Mashtaka nchini Tanzania, Frederick Kapela Manyanda alishukuru ushiriki wa wajumbe wa wataalamu wa sheria kutoka nchi za ICGLR akisema ujio wao ni neema ya kufanikisha ushirikiano dhidi ya vitendo vya kihalifu.
 Naibu Mkurugenzi Mwendesha Mashtaka nchini Tanzania, Frederick Manyanda akitoa neno la ufunguzi wakati wa mkutano wa pili wa ushirikiano wa kisheria nchi za maziwa makuu (ICGLR) unaoendelea katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam
 Mwakilishi wa Katibu Mtendaji wa ICGLR, Bi. Eliane Mokodopo akizungumza kwa niaba ya Katibu Mtendaji wa ICGLR, Balozi Zachary Muburi-Muita (hayupo pichani) wakati wa mkutano wa pili wa ushirikiano wa kisheria nchi za maziwa makuu (ICGLR) unaoendelea katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
 Mjumbe maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa nchi za Maziwa Makuu (ICGLR), Said Djinnit akizungumza wakati wa mkutano wa pili wa ushirikiano wa kisheria nchi za maziwa makuu (ICGLR) unaoendelea katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
 Balozi wa Uholanzi nchini, Mh. Jeroen Verheul akitoa salamu za taifa la Uholanzi wakati wa mkutano wa pili wa ushirikiano wa kisheria nchi za maziwa makuu (ICGLR) unaoendelea katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
 Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja (UNDP), Alvaro Rodriguez akibadilishana mawazo na mmoja wa wajumbe wa mkutano wa pili wa ushirikiano wa kisheria nchi za maziwa makuu (ICGLR) unaoendelea katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
 Kutoka kushoto ni Naibu Mkurugenzi Mwendesha Mashtaka nchini Tanzania, Frederick Manyanda, Mwakilishi wa Katibu Mtendaji wa ICGLR, Bi. Eliane Mokodopo pamoja na Balozi wa Uholanzi nchini, Mh. Jeroen Verheu wakati mkutano wa pili wa ushirikiano wa kisheria nchi za maziwa makuu (ICGLR) unaoendelea katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
  Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa nchini (UNDP), Natalie Boucly (kulia) na wajumbe wengine wakifuatilia kwa umakini hotuba mbalimbali zilizokuwa zikiwasishwa wakati wa ufunguzi wa mkutano wa pili wa ushirikiano wa kisheria nchi za maziwa makuu (ICGLR) unaoendelea katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
 Kaimu Balozi wa Marekani nchini Immi Patterson (kushoto) akiandika mambo muhimu wakati wa mkutano wa pili wa ushirikiano wa kisheria nchi za maziwa makuu (ICGLR) unaoendelea katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja (UNDP), Alvaro Rodriguez akipitia makabrasha wakati wa mkutano wa pili wa ushirikiano wa kisheria nchi za maziwa makuu (ICGLR) unaoendelea katika hoteli ya Protea Courtyard jijini Dar es Salaam.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...