*Ni baada ya kutumbukia kwenye bwawa la kuogelea la nyumbani 

Na Zainab Nyamka, Globu ya jamii

MWANAMUZIKI wa nchini Nigeria Dapo Oyebanjo ‘D’banj’ amepoteza mtoto wake wa kiume wa pekee baada ya kutumbukia kwenye bwawa la kuogelea na kufariki dunia jana nchini Nigeria.

D’banj akiwa Los Angels kwenye tuzo za muziki za BET, msanii huyo aliweza kupewa taarifa za kifo za mtoto wake anayejulikana kwa jina la  Daniel Oyebanjo III  kuwa amezama na kufa maji.

Imeripotiwa kuwa mtoto huyo, Daniel Oyebanjo III, alizama kwenye bwawa la kuogelea (swimming pool) lililopo nyumbani kwa mwanamuziki huyo huko Ikoyi, jijini Lagos.

Hivyo D’banj aliripoti kifo cha mwanaye huyo wa mwaka mmoja kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Instagram kwa kuweka picha iliyotawaliwa na rangi nyeusi ikiambatana na ujumbe uliosomeka “Nyakati ngumu, lakini Mungu wangu ni mwaminifu, wakati wote na daima.”

Imethibitishwa kuwa mke wa mwanamuziki huyo, Lineo Didi alikuwa nyumbani wakati tukio hilo likitokea na haijajulikana kama kuna mtu aliyekuwa kwenye bwawa hilo huku.

Mapema wiki hii D’ banj katika ukurasa wake wa mtandao wa Instagram ikiwa ni siku ya kina baba ‘Father’s Day’ akiwa anamvalisha mwanae pampers.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...