Na Frankius Cleophace Tarime.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilayani Tarime Mkoani Mara Marwa Daud Ngicho amechangia Kiasi Cha Shilingi Mill6 na Mifuko 100 ya Saruji kwa ajili ya Ujenzi wa Kanisa la Romani Katoliki Parokia ya Rogoro Masanga wilayani Tarime Mkoani Mara.

Ngicho amesema kuwa kama kiongozi ni wajibu wake wa kuchangia Ujuenzi wa Nyumba ya Bwana ili waumini wazidi kuombea Viongozi wanaotawala Nchi ya Tanzania na Ulimwengu akiwemo Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pome Magufuli.

“Mimi kama kiongozi nimeambatana na Wafanyakazi wangu wa Mgodini kwa ajili ya kufanikisha zoezi zima naanza kuchangia Millioni Tano na Mifuko Miamoja hapa hapa naomba Waumini wote na Viongozi kuniunga Mkono ili kufanikisha Zoezi ili” alisema Ngicho.

Mwenyekiti ameongeza kuwa Jamii inayomwamini Mwenyezi Mungu haina budi kuondokana na kuamini Miungu badala ya Mungu huku akipiga vita Waganga wanapiga ramli Chonganishi na kusema kuwa wao kama Viongozi hawatawafumbia Macho kwani wanaweza Kuchocheanakusababisha Upotevu wa Amani.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilayani Tarime Mkoani Mara Marwa Daud Ngicho akionyesha Kiasi ch Shilingi Millioni Sita Waumini wa kanisa la Rogoro katika harambee ya Ujenzi wa kanisa hilo la Romani Katoliki .
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Wilayani Tarime Mkoani Mara Marwa Daud Ngicho akikabidhi Mwenyekiti wa Parokia ya Rogoro Masanga Sebastian Siyange Kiasi cha Shilingi Millioni Sita kwa ajili ya ujenzi wa kanisa hilo.
Waumini wa kanisa la Rogoro wakiwa katika Misa takatifu kabla ya harambee hiyo.
Kanisa Jipya la Parokia ya Rogoro Masanga Wilayani Tarime Mkoani Mara linalojengwa
Viongozi mbalimbali wakiwemo Waumini wa kanisa hilo wakikagua Ujenzi wa kanisa hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...