Na Said Mwishehe, Globu ya jamii
BARAZA la Taifa la Elimu ya Ufundi(NACTE)limetengaza kufuta usajili wa vyuo 20 baada ya kubaini vimeshindwa kufuata tararibu zinazoendana na matakwa ya usajili wa vyuo hivyo.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam Kaim Katibu Mtendaji wa NACTE Dk.Adolf Rutayunga amesema uamuzi huo umefikiwa kwa kuzingatia kifungu cha 20 cha kanuni za usajili wa vyuo vya ufundi 2001.

Amesema vyuo ambavyo vimefutiwa usajili tayari baraza limeshaviandikia barua vyuo husika kuvitaka vihakikishe kuwa wanafunzi waliko kwenye programu zinazotolewa na vyuo hivyo wanahamia kwenye vyuo vingine vilivyosajiliwa na baraza kutoa programu kama hizo.

Amevitaja vyuo vilivyofutiwa usajili ni Covenant College of Business Sdudies(Dar es Salaam), Mugerezi Spatial Technology College(Dar es Salaam),Techno Brain(Dar es Salaam), DACICO Institute of Business and Management(Sumbawanga) na Arusha Institute of Technology (Arusha).

Vyuo vingine ni Lisbon Business Collage(Dar es Salaam), PCTL Training Institute(Dar es Salaam), Royal College of Tanzania(Dar es Salam), Iringa RETCO Business College(Iringa) na Highlands Health Instutute(Njombe).

Vyuo vingine ni East African Institute of Entrepreneurship and Finacial Management(EAIEFM) (Arusha), Musoma Utali Collage (Shinyanga) na Mlimani School of Professional Studies(Dar es Salaam).

Pia kuna chuo cha Dinobb Institute of Science and Business Technology(Mbeya), Institute of Social Work(Mbeya), Regency School of Hygiene (Dar es Salaam), St.Peters College of Health Sciences(Dar es Salaam), Genesis Institute of Social Science(Dar es Salaam), Institute of Management and Information Technology(Dar es Salaam) na Boston City Campus of Business College(Dar es Salaam).

Pia Dk. Rutayunga amesema mbali ya kufuta usajili kwa vyuo hivyo wamesitisha program zisizoidhinishwa na baraza ambapo vyuo vitatu vimefutiwa programu.
  Kaimu Katibu Mtendaji wa NACTE Dk. Adolf Lutayunga akizungumza na waandishi wa habari leo katika makao makuu ya NACTE Mwenge jijini Dar es salaam wakati akitangaza kufuta vyuo 20 vya ufundi ambavyo havijakidhi viwango na taratibu za usajiri uendeshaji wa vyuo nchini vya ufundi nchini kutoka kulia ni Dk. Marcelina Aloyce Baitilwake na Dk. Gema Modu Mkurugenzi wa Ushauri na Malezi ya Vyuo
Kaimu Katibu Mtendaji wa NACTE Dk. Adolf Lutayunga akizungumza na waandishi wa habari leo katika makao makuu ya NACTE Mwenge jijini Dar es salaam wakati akitangaza kufuta vyuo 20 vya ufundi ambavyo havijakidhi viwango na taratibu za usajiri uendeshaji wa vyuo nchini vya ufundi nchini kutoka kulia ni Dk. Marcelina Aloyce Baitilwake na Dk. Gema Modu Mkurugenzi wa Ushauri na Malezi ya Vyuo kulia ni Mr. Twaha A. Twaha Mkuu wa Kitengo cha Udahili NACTE.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...