TAARIFA zilizoifikia Globu ya Jamii usiku huu kutoka eneo la ajali iliyotokea maeneo ya  Riverside-Ubungo,zinaeleza kuwa gari la kubebea Wagonjwa 'Ambulance' ya Chuo kikuu cha Dar es salaam iliyokuwa ikipeleka mgonjwa Mliman Campus tokea Mabibo hostel imegongana uso kwa uso na Lori la Mizigo,habari zaidi kutoka eneno la tukio zinabainisha kuwa Watu watatu wanahofiwa kupoteza maisha,akiwemo dereva wa 'Ambulance',Nesi na Dada mjamzito anaedaiwa kuwa ni Mwanafunzi. 

Globu ya Jamii inafuatilia taarifa kamili na sahihi kwa ukaribu kabisa kutoka kwa mamlaka husika.

Mungu azilaze roho za marehemu mahali pema peponi-Amen

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...