Na Ripota Wetu,Globu ya jamii

UONGOZI wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya(NHIF) ukiongozwa na Mkurugenzi Mkuu Bernard Konga umekutana na uongozi wa Hospitali ya Benjamin Mkapa kujadili namna ya kuboresha huduma kwa wanachama wakati wanapofika kupata huduma za matibabu hosptalini hapo.

Majadiliano ya huduma kati ya watoa huduma na Mfuko yamekuwa yakifanyika kwa lengo la kuimarisha upatikanaji wa huduma kwa wanachama wa Mfuko.

Akizungumza leo kwenye kikao hicho Mkurugenzi Mkuu wa NHIF  Bw.Konga amesema kuwa suala la huduma bora kwa wanachama ni kipaumbele cha Mfuko kwa kuwa wamelipia huduma hizo kabla ya kuugua.

"NHIF na watoa huduma lazima tuwe na lugha moja ya kuwapa huduma bora wanachama wetu na kama kuna tatizo linajitokeza tulishughulikie wenyewe na sio kuwahusisha wanachama wetu.

"Na kwa kufanya hivi mwanachama atapata huduma bila usumbufu wowote na itavutia wengine kujiunga na huduma zetu," amesema Bwa.Konga.
Uongozi wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ukiongozwa na Mkurugenzi Mkuu Bernard Konga umekutana na uongozi wa Hospitali ya Benjamin Mkapa kujadili namna ya kuboresha huduma kwa wanachama wakati wanapofika kupata huduma za matibabu hospitalini hapo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...