Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera na Uratibu) Prof. Faustin Kamuzora amefurahishwa na utendajikazi wa Mfumo Unganishi wa Usimamizi wa Taarifa za Ardhi (ILMIS) unaofadhiliwa na Benki ya Dunia uliopo katika Wizara ya Ardhi Jijini Dar es Salaam.

Mradi huu utasaidia kupatikana kwa taarifa kwa urahisi na kuongeza ufanisi wa utunzaji wa taarifa za wananchi na kupunguza muda wa kutafuta taarifa kama ilivyokuwa hapo awali, alisema Prof. Kamuzora.

“Mfumo huu pia utaiwezesha Serikali kutambua walipajiwa wa ardhi, itasaidia kuboresha mazingira mazuri ya kufanya biashara na vilevile ukusanyaji wa mapato utaongezeka kwa wingi ambapo kwa sasa Mradi  huu unatekelezwa katika wilaya mbili za mfano Kinondoni na Ubungo”. Alisema Prof. Kamuzora.

Serikali imejipanga kuongeza wataalamu watakaoweza kuendesha mifumo hii pale wafadhili watakapoukabidhi ili tuumiliki na tuwezwe kuendeleza na hata kwenda kwenye mikoa mingine ili kuweza kutoa huduma za kisasa kwa wananchi.

Mapema: Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Dr. Moses Kusiluka alisema, serikali imetenga fedha ili kuweza kuwajengea uwezo wataalamu wa Tehama ili kuwezo kutumia mfumo huo pale wafadhili watakapo ukabidhi rasmi katika Wizara ya Ardhi.
Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu Sera na Uratibu  Prof. Faustin Kamuzora akizungumza baada ya kutembelea chumba kinachoanda Majadala ya usajili wa ardhi kupitia Mfumo Unganishi wa Usimamizi wa taarifa za Ardhi ( ILMIS) unaofadhiliwa na Benki ya Dunia katika Ofisi za Wizara ya Ardhi tarehe 20 Juni,2018 Jijini Dar es Salaam.
Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi na Makazi Dr. Moses Kusiluka akifafanua jambo kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Prof. Faustin Kamuzora walipotembelea chumba kinachoandaa majalada ya Msajili wa ardhi kwa kupitia Mfumo Unganishi wa Usimamizi wa Taarifa za Ardhi (ILMIS) katika Ofisi hiyo tarehe 20 Juni,2018 Jijini Dar es Salaam.
Msimamizi  wa Mradi Erick Gies Kisai akimweleza Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Prof. Faustin Kamuzora namna chumba hicho kinavyoendesha kazi za usajili wa ardhi katika Ofisi ya Wizara ya Ardhi tarehe 20 Juni,2018 Jijini Dar es Salaam.
Mratibu wa Mradi wa Kukuza Ushindani wa Sekta Binafsi (PC-PSCP) Barney Laseko akimwelezea Prof. Faustin Kamuzora namna mradi wa Mfumo Unganishi wa usimaizi wa Taarifa za Ardhi (ILMIS)  unavyofanyakazi katika Wizara ya Ardhi Tarehe 20 Juni,2018 Jijini Dar es Salaam .
Baadhi ya wafanyakazi  katika chumba cha uandikishaji wa ardhi ngazi ya kamishna wakiendelea na kazi wakati Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Prof. Faustin Kamuzora alipotembelea mradi huo tarehe 20 Juni,2018 Jijini Dar es Salaam.
Msimamizi  Uandikishaji wa Ardhi ngazi ya Kamishna Costa Chaula akimwelezea Prof. Faustin Kamuzora namna wanavyofanyakazi katika chumba hicho wakati wa ziara fupi iliyofanywa ofisini hapo tarehe 20 Juni,2018 Jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Prof. Faustin Kamuzora akipitia moja ya jalada linafanyiwa kazi katika chumba cha uandikishaji wa ardhi ngazi ya kamishna wakati wa ziara fupi iliyofanyika ofisi hapo tarehe 20Juni,2018 Jijini Dar es Salaam.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...