Mwezeshaji
wa mafunzo ya WISN PLUS POA ,Joram Kiungo toka Tamisemi akitoa somo
kwa washiriki wa mkoa wa Dar jinsi ya utoaji wa taarifa za kimfumo
katika upangaji wa watumishi katika halmashauri zao Mafunzo ya siku
mbili yaliyoanza leo mkoani mtwara na kufanyika katika kanda 6 Nchini na
kusimamiwa na tamisemi kupitia mradi wa uboreshaji wa mifumo ps 3 chini
ya ufadhili wa USAID.
Na Abdulaziz Ahmeid, Mtwara
WAKATI Serikali inatarajia kuajiri katika sekta ya
afya watumishi wapya 7680 (6180 wa Ofisi ya Tamisemi na 1500 wa Wizara ya
afya), halmashauri nchini zimetakiwa kutumia ripoti za mfumo wa WISN plus POA
iliyorahisishwa kusambaza watumishi wapya kwa kuzingatia uzito wa kazi na
mahitaji kama yalivyoainishwa kwenye taarifa hizo.
Kauli hiyo imetolewa katika kikao kazi kilicholenga
kuwasilisha matokeo ya uchambuzi wa mahitaji ya watumishi kwa kutumia mfumo wa
WISN plus POA iliyorahisishwa kinachofanyika mkoani hapa.
Mfumo wa WISN plus POA hutumika kukokotoa mahitaji
ya watumishi kwa kila kada katika vituo vya kutolea huduma kwa kuzingatia uzito
wa kazi katika kituo husika.
Meneja
mradi wa Ps 3 Mkoa wa Lindi Aloyce Mwasuka akifafanua jambo kwa
washiriki wa mafunzo hayo ya siku mbili kwa mkoa wa Dar es sallam katika
siku ya kwanza ya mafunzo hayo kwa halmashauri zote za mkoa wa Dar es
sallam baada ya mkoa wa Lindi kumaliza jana katika ukumbi wa klabu ya
bandari manispaa ya mtwara.
Kwa sasa mfumo huu unatumika kwa ajili ya vituo vya
afya na Zahanati tu, ukijumuisha kada mbalimbali zilizopo katika ngazi hizo za
utoaji huduma ambazo ni waganga (MO), waganga wasaidizi (AMO), tabibu (CO),
tabibu wasaidizi (CA), maafisa wauguzi (NO), maafisa wauguzi wasaidizi (ANO),
na wauguzi (EN).
Kikao kazi hicho pia kilitumika kuzijengea uwezo
Halmashauri na Mikoa ili ziweze kutumia WISN plus POA iliyorahisishwa kusambaza
watumishi wapya, na katika kuomba watumishi wapya.
Akizungumza katika kikao kazi hicho
kilicholenga kuwasilisha matokeo ya zoezi la kubaini mahitaji ya
watumishi kwa kutumia mfumo wa WISN PLUS POA iliyorahishwa Mganga Mkuu wa mkoa
wa Dar es salaam alisema mfumo huo ni toleo jipya unaowezesha
kutumia taarifa kutoka mfumo wa DHIS 2 kwa ajili ya kukokotoa mahitaji ya
watumishi, hivyo kupunguza gharama za kutembelea vituo kwa ajili ya kukusanya
taarifa.
Mwezeshaji
wa mafunzo ya Wisn plus Poa ,Bi Christina Godfrey ,ambae ni afisa
program ,sera na uraghibishi PS 3 akitoa elimu juu matumizi ya Tehama
ikiwa ni kuwajengea uwezo maafisa utumishi na wataalamu wa afya wa
halmashauri za mkoa wa Ruvuma juu ya namna bora ya upangaji wa
watumishi katika vituo vya kutolea huduma kwa kuzingatia mahitaji.
Kikao kazi hicho kilishirikisha Maafisa
Utumishi wa Mikoa na Halmashauri, Waganga wakuu wa wilaya, Makatibu wa Afya wa
Mikoa na Wilaya, Waratibu wa MTUHA wa Halmashauri na Wadau wa Maendeleo wa
Mradi wa PS3.
Mfumo huo ni sehemu ya Mradi wa Uimarishaji wa
Mifumo katika Sekta ya Umma – “Public Sector System Strengthening – (PS3)
unaotekelezwa kwa ufadhili awatu wa Marekani kupitia USAID.
Tayari
Halmashauri za mkoa wa lindi,Ruvuma na mtwara zimeshapatiwa mafunzo kwa
kanda ya mtwara ikifuatiwa na mikoa ya Tanga na Pwani
Bi
Restituta Masao mmoja kati ya wawezeshaji wa mafunzo kwa maafisa
utumishi wa mkoa wa Dar es sallam akitoa elimu kwa washiriki wa mafunzo
ya kuwajengea uwezo maafisa utumishi na wataalamu wa afya wa
halmashauri za mkoa huo juu ya namna bora ya upangaji wa watumishi
katika vituo vya kutolea huduma kwa kuzingatia mahitaji.
Mwezeshaji
wa mafunzo ya Wisn plus Poa ,Bi Christina Godfrey ,ambae ni afisa
program ,sera na uraghibishi PS 3 akitoa elimu juu matumizi ya Tehama
ikiwa ni kuwajengea uwezo maafisa utumishi na wataalamu wa afya wa
halmashauri za mkoa wa Ruvuma juu ya namna bora ya upangaji wa
watumishi katika vituo vya kutolea huduma kwa kuzingatia mahitaji.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...