Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Bi Anna Mghwira ametoa onyo kali kwa wakazi wa mkoa huo wanao jihusisha na uhabifu wa miundombinu ya Shirka la Umeme Tanzania (Tanesco) na kusema hatua kali zitachukuliwa dhidi yao. 

Mkuu huyo wa mkoa alisema, serikali inatumia gharama kubwa sana kuendesha shirika hilo hivyo kulihujumu kwa kuharibu miundimbinu sio sahihi na halivumiliki. 

Aliyasema hayo jana wakati akiongea na waandisi wa habari, katika kampeni maalumu inayofanywa na Tanesco makao makuu ikiwa na lengo la kuhamasisha juu ya athari za kuhujumu miumbombinu ya shirika hilo. 

“Hivi karibuni kumekuwepo na matukio ya baadhi ya watu kupoteza maisha baada ya kujaribu kujiunganishia umeme kwa njia ya wizi. naagiza wakazi wa mkoa huu kuacha kabisa tabia hiyo kwani matukio ya aina hiyo ni sawa na matukio ya uhujumu uchumi, ambayo yanarudisha nyuma jitihada za Serikali za kuhakikisha nishati ya umeme inapatikana na hivyo kufikia uchumi wa kati kupita viwanda,” alisema 

Aliongeza kuwa uhujumu wa miundombinu sio tu inaleta hasara kwa shirika lakini pia inapelekea kupoteza nguvu kazi ya taifa kupitia maafa mbalimbali ikiwemo vifo na ulemavu kwa watu wanaohusika na matukio hayo. Naye Meneja wa Tanesco Mkoa wa Kilimanjaro Mahawa Mkaka alisema changamoto ya uharibifiu wa miumbombinu unatokana na uelewa mdogo kuhusiana na madhara yatokanayo na umeme. 
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira akizungumza na waandishi wa habari katika kampeni maalumu ya kuzuia uharibifu wa miundombinu ya umeme mkoani humo. 
Meneja wa Shirika la Umeme Tanesco mkoani Kilimanjaro Mhandisi Mahawa Mkaka akizungumza na waandishi wa habari ambao hawapo pichani baadhi ya miradi inayoendelea mjini Moshi 
Meneja wa Shirika la Umeme Tanesco mkoani Kilimanjaro Mhandisi Mahawa Mkaka akiwaonyesha waandishi wa habari ambao hawapo pichani baadhi ya miradi ya umeme inayoendelea mjini Moshi pembeni ni Afisa Uhusiano wa Shirika hilo Salama
 Meneja wa Shirika la Umeme Tanesco mkoani Kilimanjaro Mhandisi Mahawa Mkaka akiwaonyesha waandishi wa habari ambao hawapo pichani baadhi ya miradi ya umeme inayoendelea mjini Moshi pembeni ni Afisa Uhusiano wa Shirika hilo Salama.
Mafundi wa Tanesco wakikata miti iliyopita katika njia za umeme Moshi. 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...