Morogoro, June 4, 2018:SERIKALI kwa kushirikikiana na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa NSSF wamejipanga kutekeleza mradi mkubwa wa Bwawa la Kidunda, hatua inayotajwa kuwa itatatua kabisa tatizo la uhaba wa maji katika jiji la Dar es Salaam katika kipindi chote cha mwaka.
Akizungumza wakati wa ziara ya ukaguzi wa mradi huo katika kijiji cha Kidunda, kata ya Mkulazi Wilaya ya Morogoro Vijijini, Waziri wa Maji na Umwagiliaji  Mhandisi Isack Kamwelwe alisema mradi huo unalenga kufanikisha adhma ya Rais John Pombe Magufuli ya kujenga uchumi wa Viwanda.
"Tunapozungumzia ustawi wa uchumi wa viwanda hususani kwa jiji la Dar es Salaam ni lazima kuwepo pia na upatikanaji wa huduma ya maji ya uhakika katika kipindi chote cha mwaka. Changamoto iliyopo sasa ni kupungua kwa kiasi cha maji katika Mto Ruvu hususani katika miezi ya Septemba na Oktoba, hivyo mradi huu unakwenda kuhakikisha mto Ruvu unakuwa na uhakika wa maji katika kipindi chote cha mwaka'' alisema.
Kwa mujibu wa Mhandisi Kamwene, mradi huo utakaotekelezwa katika kipindi cha miaka mitatu ni wazo la zamani likiwepo tangu serikali ya awamu ya kwanza chini Mwalimu Julius Nyerere na kwamba utekelezaji wake katika kipindi hiki ni mwendelezo wa adhma ya Rais Magufuli ya kutekeleza miradi mikubwa ya kitaifa.
"Kukamilika kwa mradi huu tafsiri yake ni kwamba huduma ya maji katika la Dar es Salaam inakuwa ni ya uhakika katika kipindi cha mwaka mzima'' alisisitiza.
 Waziri wa Maji na Umwagiliaji  Mhandisi Isack Kamwene (alievaa kofia ngumu) akifuatilia maelezo ya Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Maji safi na Maji Taka Dar es Salaam (DAWASA) Prof Felix Mtalo (wa pili kushoto)kuhusu mradi mkubwa wa Bwawa la Kidunda kutoka utakaotekelezwa kwa ushirikiano kati ya Serikali na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii wa NSSF alipotembelea eneo la mradi huo katika kijiji cha Kidunda, kata ya Mkulazi Wilaya ya Morogoro Vijijini mwishoni mwa wiki. Wanaoshuhudia ni pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Prof Godius Kahyarara (katikati). 
 Waziri wa Maji na Umwagiliaji  Mhandisi Isack Kamwene (kulia) akibadilishana mawazo na wadau muhimu wa mradi huo akiwemo Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Dk Stephene Kebwe (katikati), Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Prof Godius Kahyarara (wa pili kushoto) Kaimu Ofisa Mtendaji Mkuu wa DAWASA, Mhandisi Romanus Attilio Mwang'ingo (wa kwanza kushoto) wakati wa ziara hiyo.
 Waziri wa Maji na Umwagiliaji  Mhandisi Isack Kamwene (katikati) akiongozana akiongoza msafara wa wadau kuelekea eneo la mradi wakati wa ziara hiyo. Wengine ni pamoja na Mkoa wa Morogoro, Dk Stephene Kebwe (kushoto) pamoja na Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki, Omary Mgumba (kulia). 
 Baadhi ya maofisa waandamizi kutoka NSSF pamoja na DAWASA wakibadilishana mawazo wakati wa ziara hiyo.
Mchoro wa Mradi wa Bwawa la Kidunda.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...