Na Frankius Cleophacee Tarime.

Serikali imepiga vita suala la Ajira kwa watoto wadogo ikiwemo kufanya biashara ndogondogo kwa watoto hao, badala yake wapelekwe shuleni na kuahidi kuwachukulia hatua kali wazazi na walezi watakaokiuka.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Halmashari ya Wilaya ya Tarime Apoo Castro Tindwa kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Tarime Glorious Luoga katika Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika ambapo kiwilaya Wilaya ya Tarime Maadhimisho hayo yuamefanyika kwenye Viwanja vya Shule ya Sekondari Nyamongo katika Kata ya Matongo.

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Apoo Castro Tindwa amepiga vita suala la ajira kwa watoto hususani kufanya biashara ndogo katika Maeneo ya Stendi huku akipiga vita pia suala la Walimu Wa Shule za Sekondari na Msingi kufanya biashara katika Maeneo hayo.

Katika Maadhimisho hayo zimeweza kushiriki Tasisi mbalimbali Likiwemo Shirika la Jukwaa la Utu wa Mtoto CDF Tarime, ATFGM Masanga, Plan International,Muungano wa Jamii Tanzania MUJATA, Acacia North Mara pamoja na Viongozi wa Dini

Kambibi Kamugisha kutoka Shirika la Jukwaa la Utu wa Mtoto na Valerian Mgani kutoka Shirika la ATFGM Masanga wanazidi kupaza sauti zao kwa jamii ili kutokomeza Suala la Ukeketaji kwa Mtoto wa Kike Wilayani Tarime huku wakiomba serikali Kuungana na Mashirika hayo kwa lengo la kupiga Vita suala la Ukeketaji kwa Mtoto wa kike.
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Tarime Mkoani Mara Apoo Castro Tindwa akizungumza mbele ye Wananchi (hawapo pichani) wakati wa maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika,ndani ya viwanya vya shule ya sekondari Nyamongo wilayani Tarime .
Muwakilishi Kutoka Shirika la ATFGM Masanga,Valerian Mgani ambao wamekuwa wakipiga vita Ukatili katika jamii akiongea na Wananchi kwenye Maadhimisho hayo.
Muwakilishi Kutoka Shirika la Plan International , Shaban Shaban akizungumza mbele ya Wananchi katika Maadhimisho hayo.
Wanafunzi kutoka Shule za Msingi zinazozunguka Mgodi wa Uchimbaji wa Mawe ya Dhahabu ACACIA North Mara wakiwa katika Maadhimisho hayo ya Siku ya Mtoto wa Afrika,ndani ya viwanya vya shule ya sekondari Nyamongo wilayani Tarime .

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...