Sehemu ya washiriki toka vyama vya wafanyakazi, asasi za kiraia makundi ya wanafunzi na vijana uliofanyika Tarehe 7 hadi 8 jijini Dar es Salaam wakifuatilia matukio wakati wa warsha iliyojadili maswala ya usawa katika ulipaji wa kodi na manufaa yake katika kuboresha huduma za umma. 
Mmoja wa washiriki akitoa mchango wake katika warsha iliyojadili maswala ya usawa katika ulipaji wa kodi na manufaa yake katika kuboresha huduma za umma.
Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa Tanzania (TALGWU), Rashid Mtima (wa tatu kulia) akiwaongoza wajumbe wa warsha ya siku mbili iliyojadili usawa katika ulipaji wa kodi na manufaa yake katika kuboresha huduma za umma wakiimba wimbo wa ‘Mshikamano Daima’ wakati wa ufungaji wa warsha hiyo jijini Dar es Salaam. Walipendekeza serikali kupitia upya misamaha na mikataba ya kodi, kuwepo uwazi wa umiliki na faida wanazopata makampuni mbalimbali kuongeza uwezo wa TRA ili ikusanye mapato na fedha zitakazowezesha kujenga miundombinu na kuboresha huduma kwa umma. (Imeandaliwa na Robert Okanda Blogs).

HABARI ZAIDI SOMA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...