Na Nelson Nchobe wa LITA

Duniani kote taka ni kero au adha ndogo katika familia kwa sababu moja tu: katika ngazi ya kaya watu ni wachache na taka ni adha ambayo watu hao wachache wanaweza kuimudu. Ili kuondokana na kero hiyo, kwa desturi, wanakaya hukusanya taka na kuziweka eneo moja.

Lakini kaya nyingi katika mtaa au kijiji zinapokusanya taka nakuzirundika eneo moja, ubaya wa taka unapanda daraja; taka inakuwa siyo adha au changamoto ndogo tena bali taka inageuka nakuwa ni tatizo KUBWA; rundo hilo la ataka linakuwa ni jambo la hatari. Hivyo ndivyo ilivyo duniani kote.

Kwa hiyo katika nchi zote duniani ukusanyaji na uhifadhi salama wa taka vimekuwa ni tatizo sugu kwa sababu kila siku taka huzalishwa majumbani, ofisini na viwandani. Taka hizo sasa zimekuwa ni kitu cha hatari kwa uhayi wa mwanadamu na viumbe wengine. Taka zimekuwa jambo la hatari kwa sababu kimsingi taka ni uchafu na uchafu ni chanzo cha magonjwa karibu yote. Lakini si hayo tu, taka zingine ni sumu inayoharibu mazingira na kuangamiza viumbe hai, wakiwemo wanadamu.

Kwa kuwa ukusanyaji na uhifadhi salama wa taka ni tatizo la kidunia, mataifa yote yamekuwa yakihangaika ili kushinda tatizo hilo. Sasa dalili za kupambana vilivyo na tatizo hili kidunia zinaanza kuonekana mwisho wa upeo wa macho kwa sababu kuna juhudi zinazoratibika zikiongozwa na asasi ijukanayo kama Let’s Do It World chini ya taasisi iitwayo Let’s Do It Global Foundation. 

Japo ukusanyaji na uhifadhi salama wa taka nchini Tanzania bado ni ndoto, Tanzania tayari imesajiliwa na taasisi ya Let’s Do It Global Foundation kuwa ni kati ya nchi zenye dhamira ya kweli katika kupambana na taka na kulinda mazingira. Lakini kusajilika tu hakutoshi; kikubwa ni bidii ya kweli ya kukusanya na kuhifadhi salama taka zizalishwazo nchini kwa mujibu wa sheria. Afrika ina nchi 42 ambazo zimesajiliwa katika zoezi hili wanachi wan chi hizo tayari wameishapata mafunzo.

Kihistoria msukumo wa hiari wa kupambana na taka ulianzia katika nchi ndogo ya Estonia huko Ulaya mwaka 2008. Msisimko huu sasa umesambaa duniani na nchi 133 and watu takribani milioni 20 wanashiriki katika ukusanyaji wa hiari wa taka zinazozagaa sehemu zisizo rasmi au taka zilizo nje ya madapo yanayotambuliwa na mamlaka husika katika nchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...