Let's walk the talk members ...


Naomba kuwashirikisha wadau wote katika matukio yetu yajayo ya kikapu, naomba mjumuike nasi kufanikisha mashindano ya kimataifa ya kikapu ya kanda ya tano kwa timu za Taifa za vijana chini ya miaka 18 (FIBA ZoneV U18) 17-22 June 2018, yatakayofanyika hapa Dar es Salaam.
Kanda ya tano ina nchi 12 ; Egypt, Sudan, South Sudan, Eritrea , Ethiopia, Somalia, Djibouti, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi na Tanzania. Bingwa wa mashindano haya atapata tiketi ya kushiriki mashindano ya kutafuta bingwa wa Kikapu Mataifa ya Afrika (Afrobasket 2018). 
Tunahitaji fedha za kusaidia mashindano na kusaidia timu zetu za wanawake na wanaume kukaa kambini, jumla tunahitaji 100M. Corporate Sponsors karibuni na wachangiaji binafsi pia karibuni.
Makundi mbali mbali ya kijamii eg. WhatsApp groups, Telegram groups, Facebook groups, Google groups etc mnakaribishwa kuratibu na kuchanga kimakundi na mnakabidhi pamoja, Admins watakabidhi kwa niaba ya kila kikundi. 
Pamoja tunaweza, ahsanteni na Mungu awabariki wote kwa moyo wa upendo kwa vijana wetu na Taifa letu. 



Kwa mawasiliano na michango :
0713 /0784 /0767 618320. 
Phares Magesa, 
Rais, 
Tanzania Basketball Federation,

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...