SHEIKH wa Mkoa wa Tabora Ibrahim Mavumbi amemupongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa juhudi zake za kusaidia shughuli mbalimbali za kuendeleza miradi ya madhehebu mbalimbali ikiwemo  ya Waislamu hapa nchini.
Alitoa kauli hiyo mara baada ya Swala ya Eid El Fitri iliyoswaliwa Kimkoa katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi jana (leo) mjini Tabora

Sheikh Mavumbi alisema misaada anayochangia ikiwemo ya ujenzi wa nyumba za Ibada ni jambo zuri na linamuonyesha kuwa yeye sio mbaguzi  na ameonyesha mapenzi makubwa aliyonayo kwa watu wote bila kujali tofauti zao , hali inayosaidia kuimarisha umoja wa Kitaifa ulioasisiwa tangu uhuru wa Nchi ya Tanzania.

Sheikh huyo wa Mkoa aliwataka Waislamu wote nchini kuendelea kumuunga mkono Rais Magufuli na Serikali yake katika jitihada zake mbalimbali za kuwaletea wananchi maendeleo hapa nchini.

Alitoa wito kwa wakazi wote Mkoani hapa kuendelea kushirikiana na Serikali katika kudumisha mshikamano na upendo ili amani iliyopo iendelee kudumu na waumini waendelea kusali bila wasiwasi katika nyumba zao za Ibada.

Aidha Sheikh Mavumbi aliwataka Masheikh wa ngazi zote na Maimam kuhakikisha kuwa ndoa wanazofungisha zingatie maandiko matakatifu ili kuepuka kusababisha kuwepo na ndoa za utotoni mkoani humo.
 Sheikh  wa Mkoa wa Tabora Ibrahim Mavumbi (mbele) akiongoza Swala ya Eid El Fitri iliyoswaliwa Kimkoa katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi jana (leo) mjini Tabora.
 Baadhi ya Waumini wa Dini ya Kiislaam wakiwa katika Swala ya Eid El Fitri iliyoswaliwa Kimkoa katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi jana (leo) mjini Tabora.
 Baadhi wakimama wa dini ya Kiislam wakisikiliza salamu za Eid El Fitri kwa niaba ya Serikali kutoka kwa  Mkuu wa Magereza Mkoa wa Tabora Kamishna Msaidizi Mwandizi wa Magereza(SACP) Hamza Hamza (hayupo katika picha) mara baada ya Swala ya Eid El Fitri iliyoswaliwa Kimkoa katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi jana (leo) mjini Tabora.
Baadhi ya Wakinababa wa dini ya Kiislam wakisikiliza salamu za Eid El Fitri kwa niaba ya Serikali kutoka kwa  Mkuu wa Magereza Mkoa wa Tabora Kamishna Msaidizi Mwandizi wa Magereza(SACP) Hamza Hamza (hayupo katika picha) mara baada ya Swala ya Eid El Fitri iliyoswaliwa Kimkoa katika Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi jana (leo) mjini Tabora.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...