WANANCHI wa Kijiji cha Kigombe Kata ya Kigombe wilayani Muheza mkoani Tanga wametakiwa kuacha kushiriki kwenye biashara za magendo badala yake watumie maeneo yaliyorasmi kwa kisheria kwa ajili ya upitishaji wa bidhaa. 

Wito huo ulitolewa leo na Mkurugenzi wa Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa mlipa kodi Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Richard Kayombo wakati akizungumza na wananchi hao kwenye mkutano uliofanyika kwenye eneo la sokoni akiwa ameambatana na maafisa wa TRA mkoa wa Tanga. 

Alisema kitendo cha wananchi kuacha kutumia bandari ya Pangani ambayo ipo kusheria wanafanya makosa makubwa na kuwataka kuitumia kupitisha bidhaa badala ya kutumia zile ambazo hazitambuliki ambazo watakapokamatwa watafikishwa kwenye vyombo vya kisheria. 

“Tumefika hapa kigombe kutoa elimu kwa kuzungumza na wananchi kutokana na changamoto za mara kwa mara biashara za magendo ambazo zimekuwa zikipitishwa eneo hilo na kuona kutumia muda huo kuzungumza na wananchi kuwaambia madhara yake ni yapi”Alisema. 
 MKURUGENZI wa Huduma na Elimu kwa mlipa kodi Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Richard Kayombo akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Kigombe Kata ya Kigombe wilayani Muheza umuhimu wa kulipa kodi na kuacha kujihusisha na uingizaji wa bidhaa kwa njia za magendo.
 MKURUGENZI wa Huduma na Elimu kwa mlipa kodi Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Richard Kayombo akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Kigombe Kata ya Kigombe wilayani Muheza ambao hawapo pichani juu ya umuhimu wa kulipa kodi na kuacha kujihusisha na uingizaji wa bidhaa kwa njia za magendo kulia ni Kaimu Meneja wa TRA Mkoani Tanga Nazarius Mfikwa kushoto ni Mwenyekiti wa Kijiji cha Kigombe Bakari Akida Ally.
 Kaimu Meneja wa TRA Mkoani Tanga Nazarius Mfikwa akizngumza wakati wa mkutano huo kushoto ni MKURUGENZI wa Huduma na Elimu kwa mlipa kodi Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Richard Kayombo.
AFISA Mfawidhi wa Forodha Bandari ya Tanga Zahor Makame akizungumza katika mkutano huo 
Mkazi wa Kijiji cha Kigombe Kata ya Kigombe wilayani Muheza mkoani Tanga Tajiri Twaha akiuliza swali kwenye mkutano
 Sehemu ya wananchi wa Kijiji cha Kigombe kata ya Kigombe wilayani Muheza wakimsikiliza kwa umakini MKURUGENZI wa Huduma na Elimu kwa mlipa kodi Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Richard Kayombo ambaye hayupo pichani wakati alipokwenda kuzungumza nao kuhusu umuhimu wa kulipa kodi na na kuacha kujihusisha na uingizaji wa bidhaa kwa njia za magendo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...