WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka Maafisa Elimu wahakikishe wanafunzi wanaoshiriki mashindano hayo ni wale waliovuka katika ngazi ya shule, kata, wilaya na mkoa, ambao wote ni wanafunzi halali wa shule na marufuku kuchezesha mamluki.
“Endapo itabainika yupo mchezaji aliyeletwa kushiriki michezo hii ambaye si mwanafunzi (yaani mamluki) naagiza hatua kali zichukuliwe dhidi ya wahusika kwa kuzingatia kanuni na sheria za mashindano haya,” amesisitiza.
Waziri Mkuu ambaye ameambatana na mkewe Mama Mary Majaliwa ametoa agizo hilo leo (Jumamosi, Juni 9, 2018) wakati akifunguaMashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa Shule za Msingi na Sekondari Tanzania yanayofanyika kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Pia, Waziri Mkuu amewataka viongozi wa mikoa na wilaya zote nchini wahakikishe kuwa masomo ya haiba, michezo na stadi za kazi yanafundishwa kikamilifu kwenye shule zote za msingi.
Hata hivyo, Waziri Mkuu amesema somo la elimu ya michezo kwa Shule za Sekondari nalo lifundishwe kikamilifu na vyuo vya michezo kama Malya viendelee kuwaendeleza walimu wa michezo.
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akipuliza kipenga kuamuru ipigwe penati wakati
alipofungua Mashindano ya 39 ya UMISSETA na UMITASHUMTA ngazi ya Taifa
kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza Juni 9, 2018. (Picha na Ofisi
ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na wachezaji wa timu ya mpira
wa miguu ya Unguja wakati alipofungua Mashindano ya 39 ya UMISSETA na
UMITASHUMTA ngazi ya Taifa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza
Juni 9, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na wachezaji wa timu ya mpira wa
miguu ya Kagera wakati alipofungua Mashindano ya 39 ya UMISSETA na
UMITASHUMTA ngazi ya Taifa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza
Juni 9, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa na mkewe Mary (wasita kushoto) wakitazama mechi
ya mpira wa Kikapu kwa wanawake baada ya kufungua mashindano ya 39 ya
UMISSETA na UMITASHUMTA ngazi ya Taifa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba
jijini Mwanza Juni 9, 2018. Kushoto ni Naibu Waziri wa Habari,
Utamaduni, Sanaa na Michezo, Juliana Shonza na watano kushoto ni Mkuu wa
Mkoa wa Mwanza, John Mongella. Pichani, Aisha Nasoro wa Dodoma (kulia)
akimtoka Zurfa Maulid wa Singida.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na wachezaji timu ya mpira wa Kikapu
ya wanawake kutoka mkoa wa Singida wakati alipofungua Mashindano ya 39
ya UMISSETA na UMITASHUMTA ngazi ya Taifa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba
jijini Mwanza Juni 9, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri
Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipofungua Mashindano ya 39
ya UMISSETA na UMITASHUMTA ngazi ya Taifa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba
jijini Mwanza Juni 9, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Baadhi
ya wananchi wa mkoa wa Mwanza wakimsikiliza Waziri Mkuu, Kassim
Majaliwa wakati alipohutubia kabla ya kufungua Mashindano ya 39 ya
UMISSETA na UMITASHUMTA ngazi ya Taifa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba
jijini Mwanza Juni 9, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Wanafunzi
wa Shule ya Sekondari ya Wavulana ya Bwiru ya jijini Mwanza wakionyesha
halaiki kabla ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kufungua Mashindano ya 39
ya UMISSETA na UMITASHUMTA ngazi ya Taifa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba
jijini Mwanza Juni 9, 2018.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...