Na Karama Kenyunko, Globu ya Jamii
Watanzania wanaosafirisha dawa za kulevya nchini kwa njia mbali mbali ikiwemo ya kumeza tembe za dawa hizo tumboni kwa dhumuni ya kuzipeleka nje ya nchi au kufanyabiashara hiyo haramu ndani ya nchi wameaswa kuacha vitendo hivyo mara moja la sivyo wakikamatwa na kutiwa hatiani adhabu kali ikiwemo kifo itawakabili.

Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa, amesema hayo leo Juni 26, 2018 wakati wa maadhimisho ya kitaifa ya siku ya kupiga vita dawa za kulevya duniani iliyofanyika mkoani Iringa.

Amesema, Tanzania kama mwanachama wa umoja wa mataifa haina budi kuuungana na mataifa mengine duniani kutekeleza malengo ya umoja huo ya maendeleo endelevu ili ifikapo mwaka 2030 kwa kupiga vita matuimizi na biashara hiyo haramu ili kujenga maisha yetu, jamii yetu na utu wetu bila dawa za kulevya.

Waziri Majaliwa pia amewaonya wananchi kutojihusisha kabisa na matuimizi wala biashara ya dawa za kulevya, kwani biashara hiyo haramu haikubaliki duniani na hata dini zote zinaipinga vikali, kwani kutumia dawa za kulevvya ni kujiletea laana kubwa kutoka kwa muumba.
Alizataja dawa za kulevya zilizobainika kutumiwa kwa wingi hapa nchini ni bangi, heroine na cocaine ambazo hutumiwa zaidi na vijana wa kuanzia umri wa miaka 15 hadi 35 ambapo utafiti uliofanywa na wizara ya afya mwaka 2014 unaonesha kuwa vijana kati ya 250,000 hadi 500,000 hutumia heroine na kati yao, vijana 300,000 hutumia dawa dawa hiyo kwa njia ya kujidunga.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na wananchi wa mkoa wa Iringa wakati wa maadhimisho ya kitaifa ya siku ya kupambana na dawa za kulevya Duniani yaliyofanyika katika kiwanja cha Kichangani mkoani Iringa leo.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipeperusha bendera aliyokabidhiwa na wananchi waliofanya matembezi ya kutoa elimu kwa wananchi yaliyofanyika kwa siku tatu mkoani Iringa wakati wa maadhimisho ya kitaifa ya siku ya kupambana na dawa za kulevya Duniani.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea bendera kutoka kwa wananchi waliofanya matembezi ya kutoa elimu kwa wananchi yaliyofanyika kwa siku tatu mkoani Iringa wakati wa maadhimisho ya kitaifa ya siku ya kupambana na dawa za kulevya Duniani yaliyofanyika katika kiwanja cha Kichangani mkoani Iringa leo.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa(katikati) akiwapungia mikono wakati alipokuwa anapokea maandamano ya wananchi pamoja na wadau mbalimbali wa kupambana na dawa za kulevya wakati wa maadhimisho ya kitaifa ya siku ya kupambana na dawa za kulevya Duniani yaliyofanyika katika kiwanja cha Kichangani mkoani Iringa leo. Kulia ni Mkuu wa mkoa wa Iringa, Amina Masenza na kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu) Mh. Jenista Mhagama.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa(kulia) akizungumza jambo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Kazi, Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu) Mh. Jenista Mhagama wakati wa maadhimisho ya kitaifa ya siku ya kupambana na dawa za ulevya Duniani yaliyofanyika katika kiwanja cha Kichangani mkoani Iringa leo.


Baadhi ya wananchi pamoja na wadau wa kupambana na dawa za kulevya wakipita kwa bashasha mbele ya mgeni rasmi wakati wa maadhimisho ya kitaifa ya siku ya kupambana na dawa za kulevya Duniani yaliyofanyika katika kiwanja cha Kichangani mkoani Iringa leo.

Baadhi ya viongozi wa serikali na wananchi wa wa mkoa wa Iringa wakiwa kwenye maadhimisho ya kitaifa ya siku ya kupambana na dawa za kulevya Duniani yaliyofanyika katika kiwanja cha Kichangani mkoani Iringa leo.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Kamishna wa Sheria Edwin Kakolaki alipotembelea banda la mamlaka ya kudhibiti na kupambana na Dawa za Kulevyawakati wa maadhimisho ya kitaifa ya siku ya kupambana na dawa za kulevya Duniani yaliyofanyika katika kiwanja cha Kichangani mkoani Iringa leo.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...