Na George Binagi-GB Pazzo, BMG 
Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa amesema hali ya kiwango cha michezo nchini si ya kuridhisha hivyo lazima wanamichezo kuanzia shule za awali, msingi, sekondari pamoja na vyuo waandaliwe vyema. 
 Waziri Majaliwa aliyasema hayo jana katika uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza wakati akifungua rasmi Mashindano ya Umoja wa Michezo kwa shule za Sekondari nchini UMISSETA, ulioambatana na pia na ufunguzi wa mashindano ya Umoja wa Michezo na Taaluma kwa shule za Msingi UMITASHUMTA. 
 Mkuu wa Mkoa Mwanza Mhe.John Mongella alitoa pongezi kwa viongozi na wadau wote wakiwemo wadhamini wakuu kampuni ya Cocacola kwa kufanikisha maandalizi ya michezo ya UMISSETA na UMITASHUMTA inayofanyika kwa mwaka wa tatu mfululizo Jijini Mwanza ambapo mwakani michezo hiyo itafanyika Jijini Dodoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...