*Ataja hatua ambazo wanazochukua kukabiliana nao kote nchini 
*Akiri kuripotiwa homa ya Chikungunya,  Dengue katika Jiji la Dar 

Na Said Mwishehe,Globu ya jamii

WAZIRI wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amesema hakuna ugonjwa wa Ebola nchini ila kuna hatari ya kuupata.

Hivyo amewahakikishia Watanzania kutokuwa na hofu ha kueleza Serikali imeshachukua hatua mbalimbali za kukabiliana na ugonjwa huo ikiwa ni pamoja na kuweka mashine za kupima ugonjwa huo katika mipaka yote nchini na kuweka vituo vya matibabu kote kila mkoa.

Waziri Mwalim ametoa kauli hiyo leo jijini Dar es Salaam wakati anazungumzia homa ya Chikungunya na Dengue ambapo amekiri kuwepo kwa wananchi waliougua magonjwa hayo.Kuhusu Ebola amesema hawajapokea wala kupata  taarifa za mtu yoyote kuugua ugonjwa huo nchini.

"Hatuna mgonjwa wa Ebola ila tupo katika nchi sita ambazo zipo hatarini kupata ugonjwa huo kutokana na kupakana na nchi ya Congo ambayo  iripotiwa watu 43 kuugua Ebola."Pia kuna muingiliano mkubwa wa watu nchini kwetu.Hivyo kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) tupo hatarini kuupata,"amefafanua.

Waziri Mwalim amesema Wizara ya Afya na Serikali kwa ujumla tayari wamejipanga kukabiliana na Ebola kwa kuchukua hatua mbalimbali ikiwamo kuunda timu maalum ya kufuatilia.Pia wametenga maeneo ya kutoa huduma za afya kila mkoa iwapo kutabainika kuna mgonjwa wa Ebola amebainika iwe rahisi kupatiwa matibabu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...