*Ni kwa kitendo cha Wizara kuingia mgahawa wa Bunge kupima samaki
*Amwambia Waziri Mkuu kilichofanyika si uungwana, akubali kusamehe yaishe

Na Said Mwishehe,
wa Globu ya jamii

PAMOJA na Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina kuliomba radhi Bunge kwa kitendo cha Wizara yake kuingia kwenye mgahawa wa Bunge bila kibali na kupima samaki waliopikwa kwa rula, Spika wa Bunge Job Ndugai amasema kitendo hicho ni udhalilishaji.

Juzi Waziri Mpina alitoa maagizo kwa watendaji wa Wizara yake kuingia kwenye Mgahawa wa Bunge na kisha kuingia jikoni kupima samaki ambao tayari walikuwa wamepikwa.Kitendo hicho kilisababisha wabunge kuchachama na kutoa hoja ili kujadili kitendo hicho.Mbunge Peter Serukamba ndio aliyeomba muongozo.
Hivyo leo Mpina akiwa bungeni mjini Dodoma ameomba radhi Bunge pamoja na Spika wa Bunge kwa kitendo hicho.Hata hivyo Spika Ndugai amemueleza Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kuwa kitendo hicho ni udhalilishaji na si sahihi."Tunamshukuru Waziri kutokana na maelezo ambayo ameyatoa lakini niseme tu kwa Waziri Mkuu tumesikitishwa na kilichotokea.
"Sisi si Bunge pekee duniani bali ni sehemu ya mabunge mengine ya jumuiya ya madola.Ikisikika kuna Waziri amefanya kitendo hiki bungeni ni kosa. "Hata kama kuna kosa la jinai ambalo limefanyika ndani ya Bunge ni vema Spika akajulishwa badala ya watu kuingia tu,"amesema Spika Ndugai.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...