Ramadhani Ali – Maelezo Zanzibar
Wakala wa Chakula na Dawa  Zanzibar (ZFDA) imezuia kusambazwa bidhaa za chakula na vipodozi zilizoingizwa nchini kwa ajili ya mwezi mtukufu wa Ramadhani na siku kuu ya Idd el Fitri kinyume na taratibu na zilizokuwa hazifai kwa matumizi ya binadamu.

Mkurugenzi Mtendaji wa ZFDA Dkt. Burhan Othman Simai alisema bidhaa hizo zilikamatwa kufuatia operesheni maalumu waliyoifanya katika kipindi cha miezi miwili kwenye maghala ya wafanyabiashara na baadhi ziligundulika zimetupwa katika jaa la Kibele na eneo la Migombani.

Akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake Mombasa Dkt. Burhani alizitaja bidhaa zilizokamatwa na zilizotupwa kuwa ni mchele tani 40, unga wa sembe tani 75,  sukari tani 25 na lita 15,000 za mafuta ya kula.

Alisema dawa na vipodozi vilivyokamatwa ni vichupa 4000 vya chanjo aina ya ATS kutoka China zilizoingizwa nchini kinyume na miongozo ya uingizaji na utoaji wa dawa nchini, na tani tisa za vipodozi vyenye viambata vya sumu kali inayosababisha saratani ya ngozi.

Dkt. Burhan alieleza masikitiko yako kwa baadhi ya wafanyabiashara kutoa sadaka bidhaa hizo bila kuangalia athari inayoweza kuwapata wananchi wenzao baada ya kuzitumia.
MKURUGENZI Mtendaji Bodi ya Chakula na Dawa Zanzibar, Dkt. Burhan Othman Simai (kulia) akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na zoezi la Kukamata bidhaa zisizofaa kwa matumizi ya Binaadamu miezi miwili iliyopita. 
 Mkuu wa Ukaguzi wa Chakula Mohammed Shadhil (kushoto) na Muangalizi wa Ofisi Mussa Bakar Othman wakionesha  vipodozi vyenye chemicali za sumu zilizoingizwa kwa ajili ya siku kuu
Aina za Bidhaa za Mchele, Unga wa Ngano,Mafuta ya Kula na vipodozi zilizokamatwa na ZFDA ambazo  hazifai kwa  matumizi ya Binaadamu.
Picha na Abdalla omar Maelezo – Zanzibar.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...