Na Agness Francis, Globu ya jamii
Azam fc yatamba kumgaragaza mnyama simba katika fainali za kuwania kombe la kagame cup (cecafa).
Timu hizo zote mbili za kutoka hapa nchini ambazo zimefanikiwa kutinga fainali zitashuka dimbani kesho majira ya saa 12 jioni kuchoshana nguvu katika uwanja wa taifa Jijini Dar es Salaam.
Mara baada ya jana azamfc kumuondosha gor mahia ya nchini kenya katika michuano hiyo kwa kipigo cha mabao 2-0, sasa wanakutana na wekundu wa msimbazi katika kumjua nani ataibuka kidedea wa kombe hilo.
Akizungumza leo jijini Dar es salaam msemaji wa Azam FC Jaffary Iddi Maganga amesema kuwa kikosi chao kimejipanga vizuri kuhakikisha wanatetea ubingwa wao wa mwaka 2015 ambapo michuano hiyo ilifanyika kwa mara ya mwisho hapa nchini.
Jaffary amesema maandalizi waliyofanya ni mazuri na ndio maana wamefanya vema na mpka kufikia hatua hiyo.
"Tunaiheshimu simba ni timu kongwe ya muda mrefu ilio na kikosi mahiri lakini sisi azam tunaliamini benchi letu la ufundi pamoja na mwalimu,tunaahidi kufanya vizuri kwa kumfunga simba"amesema jaffary.
Mtanange huo utakaokuwa wa ina yake wa kiburudani kwa mashabiki ,inaonyesha zahiri kuwa soka la Tanzania limezidi kuimarika katika ukanda huu wa Afrika mashariki na kati.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...