Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Hati za utambulisho kutoka kwa Balozi mteule wa Kenya hapa nchini Dan Kazungu Ikulu jijini Dar es Salaam leo Julai 30, 2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika mazungumzo Balozi mteule wa Kenya hapa nchini Dan Kazungu  mara baada ya kuwasilisha Hati zake za Utambulisho Ikulu jijini Dar es Salaam leo Julai 30, 2018
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea zawadi ya Picha kutoka kwa Balozi mteule wa Kenya hapa nchini Dan Kazungu. Zawadi hiyo ya picha imetoka kwa Mama mzazi wa Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta, Mama Ngina Kenyatta na katika picha hiyo anaonekana Rais Dkt. Magufuli akiwa na Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta pamoja na Mama Ngina Kenya walipokuwa Nairobi nchini Kenya.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi Balozi wa  Kenya nchini Mhe. Dan Kazungu  hati ya kiwanja cha  kujengea mjini Dodoma kwenye hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Julai 30, 2018
 Balozi wa  Kenya nchini Mhe. Dan Kazungu  akielekea kuketi baada ya kupatiwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Magufuli hati ya kiwanja cha  kujengea mjini Dodoma kwenye hafla iliyofanyika ukumbi wa mikutano wa Kikwete Ikulu jijini Dar es salaam leo Julai 30, 2018. Hii ilikuwa kazi ya kwanza kwa balozi huyu ambaye alijiunga na wenzie baada ya kukabidhi hati za utambulisho kwa Rais muda mfupi uliopita.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...