Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amewashauri Wana Habari wa Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC) kuendelea kuwa wabunifu zaidi wa vipindi vitakavyoleta mvuto na hatimae kuwa na wasikilizaji wengi zaidi wa Shirika hilo Nchini.
Alisema licha ya kuwepo kwa vipindi vingi vilivyokuwa maarufu na kukubalika kwa wasikiizaji wengi akitolea mfano Kipindi cha Mawio na Maelezo baada ya Habari lakini bado juhudi za ubunifu zinahitajika katika kuona Mfumo wa Matangazo unawafikia Wananchi wengi zaidi Mjini na Vijijini.
Balozi Seif Ali Iddi alitoa ushauri huo wakati alipofanya ziara fupi katika Kituo cha Matangazo cha Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC – REDIO) kiliopo Rahaleo Mjini Zanzibar kuangalia shughuli za utendaji kazi wa Taasisi hiyo ya Habari na kuridhika na jitihada zinazochukuliwa na Watendaji wawake.
Alisema upo umuhimu wa vipindi na matangazo ya ZBC Redio kuangaza zaidi kwa upande wa Majimboni na Vijijini ili Wananchi wa maeneo hayo wawe na fursa ya kuwasilisha changamoto zinazowakabili hasa katika harakazi zao za kujiletea maendeleo.
Balozi Seif alieleza kwamba wakati Serikali Kuu inafikiria jitihada za kusaidia changamoto zinazowakabili watendaji wa Kituo hicho cha Matangazo ya Radio ambapo pia kupitia nafasi yake ya Uwakilishi atajaribu kuwashawishi Wawakilishi wenzake majimboni kutoa ushirikiano utakaowezesha kuendelezwa kwa Vipindi vya kutoka Majimboni.
Alisema vipo vipindi vinavyoweza kusaidia Wananchi kuelimika zaidi ambavyo vinapaswa kupewa umuhimu wa pekee ili kupunguza kero zinazowakabili sambamba na kumrahisishia Mwakilishi kutekeleza majukumu yake badala ya kusubiri Vikao vya Baraza la Wawakilishi.
Makamu
wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akilakiwa na Naibu
Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utalii na Mambo ya Kale anayesimamia
Habari Dr. Yussuf Mnemo alipofanya ziara fupi katika Kituo cha
Matangazo cha Shirika la Utangazaji Zanzibar (ZBC – REDIO). Kulia ya Dr.
Mnemo ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Zanzibar Bibi Iman
Duwe na Naibu Wake Bibi Nasra Mohamed.
Msaidizi
Mhariri Mkuu wa Chumba cha Habari ZBC –Redio Amour Nassor akimuelezea
Balozi Seif aliyepo (katikati) Majukumu ya Wana Habari katika
uwajibikaji wao wa kila siku. Wa kwanza kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa
ZBC Bibi Iman Duwe nas kushoto ya Balozi Seif ni Naibu Waziri wa Nchi
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mh. Mihayo Juma N’hunga.
Fundi
Mkuu wa Shirika la Utangazaji Zanzibar Ali Boud Talib aliyevaa kofia ya
Kiua akimpatia maelezo balozi Seif ndani ya moja ya Studio ya
Watangazaji wakati wa ziara yake katika Kituo cha Matangazo ya Redio
Rahaleo. Wa kwanza kutoka Kushoto ni Mtangazaji mahiri wa Redio na
Televisheni Khamis Mohamed na Mkuu wa Kitengo cha Watangazaji Bibi Suzan
Peter Kunambi.
Mtangazaji
wa Spice FM ambae pia mpiga picha wa ZBC – TV Said Golo na watangazaji
wenzake wakifurahia ujio wa Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi
Seif Ali Iddi ndani ya Studio yao iliyopo Rahaleo.
Balozi
Seif akisisitiza umuhimu wa Uongozi wa ZBC kutumia Bajeti zao za Mwaka
katika kutanzua baadhi ya changamoto zinazowakabili ikiwemo Vikalio.
Picha na – OPMR – ZNZ.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...