CHAMA Cha Mapinduzi(CCM) kimekabidhi gari la kubeba wagonjwa katika Kata ya Leng'ata wilayani Mwanga mkoani Kilimanjaro.
Kukabidhiwa kwa gari hiyo ni moja ya mkakati wa CCM wa kuendelea kutekeleza ahadi ya kuboresha na kusogeza huduam za afya karibu na wananchi kwa kufanikisha kupatikana kwa gari hiyo.
Gari hiyo imekebidhiwa jana katika kituo cha afya cha Kagongo ambapo Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Humphrey Polepole ndio aliyekabidhi kwa niaba ya Rais John Magufuli ambaye ndiye aliyetoa gari hilo baada ya kupokea kilio cha wananchi kupitia Mbunge wa Jimbo la Mwanga Proesa Jumanne Maghembe
Akizungumza baada ya kukabidhi gari Polepole amesema Rais Magufuli anawapenda wananchi wote bila kubagua vyama vyao."Na CCM nayo inahimiza utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2015 mpaka 2020 hata katika maeneo yanayoongozwa na upinzani ndio maana gari la kubebea wagonjwa limetolewa katika Kata yenye Diwani wa upinzani ili kuendeleza dhana ya CCM kuwa maendeleo yanayotolewa na Serikali ya CCM hayana chama,"amesema.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...