JOSEPH MPANGALA

Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi wa Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za wanyonge Tanzania MKURABITA,Balozi Daniel Ole Njoolai ameiomba Halmashauri kote nChini Kuhakikisha zinasaidia Mpango wa kurasimisha ardhi ili wananchii waweze kupatiwa hati zitakazowawezesha kujikwamua kiuchumi.

Hayo yameyasema katika makabidhiano ya uongozi wa Kamati Hiyo ambayo ilikuwa ikiongozwa na Kaptein Mstaafu John Chiligati katika kipindi cha Miaka Mitatu Jijini Dodoma.

Balozi Njoolay amesema katikakipindi chake cha uongozi kama mkuu wa mkoa kwa miaka 16 tayari anazifaham Halmashauri hivyo kuziomba kushirikiana ili kuwezesha Wananchi kuweza kurasimisha ardhi na Biashara.

“Mimi nimefanyakazi kama mkuu wa Mkoakwa Miaka 16 Nazifaham Halmashauri,Nitumia nafasi hii kuziomba Halmashauri Zitusaidie sana,ziwe positive kwa swala hili watu wao ndio Tunawasaidia kwa sababu Bila halmashauri hakuna Kitu”amesema Balozi Njoolay

Naye Mwenyekiti Mstaafu wa kamati hiyo Kaptein Mstaafu John Chiligati amesema wananchii wa Vijijini ambao wanakadiriwa kufikia asilimia 80 hawana uwelewa wa Urasimishaji ingawa wanamashamba Makubwa lakini hayana hati ya Umiliki hivyo kuendelea kubaki kuwa masikini.

“Wananchii wetu wa Vijijini karibu asilimia 80%mtu ambaye anamigomba yake mihogo yake kila kitu anacho halafu anasema masikini wakati Duniani kote Mtu ambaye anamiliki Ardhi anaitwa LandLord yaan ni mtu ambaye yuko vizuri lakini siri yake ni kwamba hii mali aliyonayo bado haitambuliki na yeyote”Amesema Chiligati Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za wanyonge Tanzania MKURABITA Ulianzishwa mwaka 2004 na tayari umefika katika mikoa 27,23 mikoa ya Tanzania Bara na mikoa 4 ya Zanzibar na tayari hati hati elf 71 na 51 na zimewawezesha kukopa shilingi Billlion 5.5 kutoka katika taasisi mbalimbali za kifedha
Mwenyekiti Mstaafu wa Kamati ya Uongozi ya Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za wanyonge Tanzania (MKURABITA), Kapteni Mstaafu John Chiligati akimkabidhi kitabu cha mwongozo, Mwenyekiti mpya wa Kamati hiyo, Balozi Daniel Ole Njoolay mbele ya wajumbe na watendaji wa kamati hiyo jijini Dodoma.

Mwenyekiti mpya wa Kamati ya Uongozi ya Mpango wa Kurasimisha Rasilimali na Biashara za wanyonge Tanzania (MKURABITA), Balozi Daniel Ole Njoolay akizunguza mbele ya watendaji na jumbe wapya MKURABITA katika kikao elekezi kilichofanyika jijini Dodoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...