Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
TAFITI zote lazima ziombewe vibali kabla ya kuanza kufanya utafiti huo ikiwa kuhakikisha tafiti zinakuwa na viwango vinavyoendana taratibu zilizowekwa na Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (Costech)
Akizungumza katika Maonesho Mkutubi wa Costech Amedeus Maro amesema kuwa mtu akipata kibali cha kufanya utafiti baada ya kukamilika lazima apeleke kabla kwenda katika matumizi mengine.
Amesema kuwa kunatofauti kati tafiti za kitaaluma na tafiti kwa ajili ya kutumika katika umma ambazo zinahitajika kuangaliwa njia zilizotumika kwa kuangalia masilahi mapana ya umma.
Amesema kuwa zinazofanywa na vyuo mwenye dhamana ni mkuu wa Chuo ndiye anayetambulika na Costech na wanafunzi wa nje ya nchi wanaotaka kufanya utafiti lazima waombe Costech kutokana kuwa hakuna mahusiano na mkuu wa chuo cha nje ya nchi.
Maro amesema kuwa wananchi na watafiti kuweza kufanya mawasiliano na Costech kabla ya kufanya utafiti na bila kufanya hivyo hatua kali atachukuliwa kwa mtu atakayefanya utafiti.
Afisa wa Tehama wa Costech Alfred Nyoni akizungumza na wananchi waliotembelea banda la Costech katika Maonesho ya Vyuo Vikuu yanayofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Meneja wa Miradi wa Magilatech , Godwin Mloka akizungumza na wananchi kuhusiana na ugunduzi wa technolojia Maonesho ya Vyuo Vikuu yanayofanyika katika Viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...