Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii

MKUU wa Wilaya ya Ilala jijini Dar es Salaam Sophia Mjema amezindua rasmi semina ya wanawake wajasiriamali ijulikanayo kama Changamka Mwanamke ambayo imehusisha maonesho ya bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa na vikundi vya akina mama katika Wilaya hiyo.

Akizungumza leo katika hafla hiyo Mjema amesema kuwa  jukwaa hilo lenye lengo na nia ya kuwakwamua wanawake linajitosheleza, hivyo hakuna mwanamke atakayebaki kama alivyo mara baada ya kumalizika kwa semina hiyo.

Amewahimiza  na kuwa na jitihada katika kuhakikisha malengo yao yanatimia. Ameeleza kuwa amefurahishwa na shughuli zinazofanywa na wanawake hao kwani wameanzisha viwanda vidogo ambapo serikali ya awamu ya tano ina mlengo huo.

Mjema amewahaidi kuwashika mkono na kushirikiana nao ili kuweza kufikia uchumi wa  kati. Pia amesema kuwa kuna mifuko 19 ya kuwawezesha wanawake katika kila sekta na amewataka wanawake kuwekeza katika sekta mbalimbali.

Ametaja baadhi ya sekta hizo ni ufugaji, uvuvi, kilimo na nyinginezo na mikopo ya asilimia 20 itatolewa kwa akina mama, 20 kwa vijana na asilimia 10 kwa wazee na hii ni katika kuhakikisha uchumi wa wanawake na taifa unakua imara.
 Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema akikagua moja ya bidhaa zinazotengenezwa na wanawake wajisiriamali katika uzinduzi wa semina hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema akipata maelezo ya namna bidhaa hizo zinavyozalishwa alipokuwa katika moja ya mabanda ya wajasiriamali hao.

 Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema akizungumza na waandishi wa habari wakati wa hafla ya uzinduzi wa semina ya wajasiriamali leo jijini Dar es salaam

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...