Na.Vero Ignatus .Dodoma. 

Taasisi ya RSA kwa kushirikiana na Jeshi la polisi kikosi cha usalama barabarani kimefanya ukaguzi wa magari yanayoingia na kutoka stendi kuu ya mabasi mkoani Dodoma nanenane.

Ukaguzi huo umeenda sambaba pamoja na kutoa elimu kwa abiria namna ya kufunga mikanda awapo ndani ya gari,kuzifahamu haki zao za msingi pamoja na kupaza sauti kutokaa kimya pale anapomuona dereva anakiuka sheria na taratibu za usalama barabarani

John Seka ni mwenyekiti wa RSA nchini amesema Imekuwa ni tabia ya Taasisi hiyo kufanya hivyo mara kwa mara ili kuwakumbusha madereva wajibu wao,kufuata taratibu na kanuni za usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazosababishwa madereva wazembe .

"Tumejaribu kupenyeza elimu kuhusu maswala ya usalama barabarani na tumefanya hivyo kwasababu ajali zimekuwa zikiongezeka kila siku,hivyo tumeona na sisi kama RSA kuna umuhimu wa kupaza sauti kwaajili ya usalama barabarani"

Askari wa kikosi cha usalama barabarani wankituoncha mabasi mkoani Dodoma Koplo Athuman amewataka RSA kuendelea kushirikiana na Jeshi la polisi katika kutoa taarifa, pale wanapoona mwenendo mbaya wa madereva wawapo barabarani kwani itasaidia kupunguza ajali.Sisi askari hatupo mahali pote ila nyie RSA mkitupa taarifa tutazitendea kazi,endeleeni kutoa elimu kwa abiria na kwa madereva hii itasaidia kupunguza ajali.Alisema Athumani.

Katika ukaguzi huo uliofanyika katika stendi hiyo ya mabasi makosa mbalimbali yamegundulika likiwemo la baadhi ya mabasi kuwaongezea abiria nauli,magari kukosa mikanda,pamoja na baadhi ya magari kuktwa na ubovu mbalimbali.
Baadhi ya mabalozi wa Usalama barabarani wakiwa katika stendi kuu ya mabasi mkoani Dodoma.
Meneja wa TIRA Kanda ya Kati Stella Rutaguzaal akizungumza na mabalozi wa usalama barabarani leo Mkoani Dodoma
Mmoja wa askari wa kikosi cha usalama barabarani akimsaidia mmiliki wa mabasi ya Kamwana Nassoro Khlfani

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...