Mbunge wa Songea Mjini Dr. Damas Ndumbaro akizungumza wakati wa kufunga mashindano ya Vilabu vya Kodi kwa shule za Sekondari katika Tamasha la Majimaji Serebuka 2018 linaloendelea Mkoani Ruvuma. Wengine kutoka kushoto ni Meneja wa TRA mkoa wa Ruvuma Rosalina Mwenda, Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa TRA Richard Kayombo na Meneja wa NMB Ruvuma Ritha Majahasi.
 Mwanafunzi kutoka shule ya Sekondari Londoni akipongezwa na Mbunge wa Songea Mjini Dr. Damas Ndumbaro (wa pili kulia) baada ya shule yake kuibuka mshindi wa jumla wa mashindano ya Vilabu vya Kodi kwa shule za Sekondari katika Tamasha la Majimaji Serebuka 2018.
  Mwanaidi Hamisi mwanafunzi wa shule ya Sekondari Maposeni akipokea zawadi ya kibubu baada ya kuibuka mshindi wa pili katika shindano la uchoraji wa kibonzo kinachohusu masuala ya kodi.
Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa TRA Richard Kayombo akimkabidhi kibubu ambacho ameweka fedha taslim shilingi 50,000 mmoja wa wanafunzi walioibuka washindi wa kuwasilisha vizuri mada kuhusu mashine za kodi za kielektroniki wakati wa mashindano ya Vilabu vya Kodi kwa shule za Sekondari  katika Tamasha la Majimaji Serebuka 2018.
 Washindi wa jumla wa mashindano ya Vilabu vya Kodi kwa Shule za Sekondari katika Tamasha la Majimaji Serebuka 2018 (waliosimama) wakiwa katika picha ya pamoja na Mbunge wa Songea Mjini Dr. Damas Ndumbaro (wa pili kulia), Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa TRA Richard Kayombo (wa pili kushoto), Meneja wa TRA Ruvuma Rosalina Mwenda (wa kwanza kushoto) na Meneja wa NBM Ruvuma Ritha Majahasi (wa kwanza kulia).

 Majaji (waliosimama) walioshiriki kuchagua shule bora na wanafunzi bora katika mashindano ya Vilabu vya Kodi kwa shule za Sekondari katika Tamasha la Majimaji Serebuka 2018 wakiwa katika picha ya pamoja na Mbunge wa Songea Mjini Dr. Damas Ndumbaro (wa pili kulia), Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa TRA Richard Kayombo (wa pili kushoto), Meneja wa TRA Ruvuma Rosalina Mwenda (wa kwanza kushoto) na Meneja wa NBM Ruvuma Ritha Majahasi (wa kwanza kulia).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...