Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewapongeza wakazi wa Wilaya ya Mbozi kwa kujiunga kwa wingi katika huduma ya Bima ya Afya ambapo zaidi ya asilimia 77% ya wananchi wa mkoa wa Songwe wamejiunga na huduma hiyo ya bima.
Makamu wa Rais ameyasema hayo leo wakati akihutubia wakazi wa kata ya Iyula kwenye viwanja vya mikutano vya Iyula B ikiwa siku ya pili ya ziara yake ya siku 5 mkoani Songwe.
Makamu wa Rais ametoa rai kwa wananchi wa wilaya ya Mbozi kujikinga na ukimwi ambapo aliwaambia kila mwananchi anawajibu wa kujilinda mwenyewe.
Aidha Makamu wa Rais amepongeza wananchi kwa kuitikia wito wa chanjo ambapo zaidi ya ailimia 80% ya chanjo imechanjwa kwa mama na mtot0.
Mapema leo, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alifungua kituo cha Afya cha Nanyala kilichogharimu shilingi milioni 820 ambapo wakazi zaidi ya elfu kumi kutoka vijiji vitano katika kata ya Nanyala watapata hudumua na kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa mradi wa maji Iyula ambao utawasaidia zaidi ya wananchi 46,000.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Makamu wa Rais ameyasema hayo leo wakati akihutubia wakazi wa kata ya Iyula kwenye viwanja vya mikutano vya Iyula B ikiwa siku ya pili ya ziara yake ya siku 5 mkoani Songwe.
Makamu wa Rais ametoa rai kwa wananchi wa wilaya ya Mbozi kujikinga na ukimwi ambapo aliwaambia kila mwananchi anawajibu wa kujilinda mwenyewe.
Aidha Makamu wa Rais amepongeza wananchi kwa kuitikia wito wa chanjo ambapo zaidi ya ailimia 80% ya chanjo imechanjwa kwa mama na mtot0.
Mapema leo, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alifungua kituo cha Afya cha Nanyala kilichogharimu shilingi milioni 820 ambapo wakazi zaidi ya elfu kumi kutoka vijiji vitano katika kata ya Nanyala watapata hudumua na kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa mradi wa maji Iyula ambao utawasaidia zaidi ya wananchi 46,000.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan leo
amefungua kituo cha Afya cha Nanyala kilichopo kata ya Nanyala wilayani
Mbozi kitakachotoa huduma kwa wakazi zaidi ya elfu kumi ikiwa siku ya
pili ya ziara yake ya siku 5 katika mkoa wa Songwe. Pichani kulia ni
Mkuu wa Mkoa wa Songwe Mh.Chiku Galawa. (Picha na Ofisi ya Makamu wa
Rais)
Muonekano
wa jengo la kituo cha Afya cha Nanyala kilichopo kata ya Nanyala
wilayani Mbozi kitakachotoa huduma kwa wakazi zaidi ya elfu kumi
Jiwe la Msingi lililowekwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
Baadhi
ya Wananchi wakimsikiliza Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan (hayupo pichani) alipokuwa
akiwahutubia mapema leo mara baada ya kufungua kituo cha Afya cha
Nanyala kilichopo kata ya Nanyala wilayani Mbozi kitakachotoa huduma kwa
wakazi zaidi ya elfu kumi ikiwa siku ya pili ya ziara yake ya siku 5
katika mkoa wa Songwe. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
akiwahutubia Wananchi mapema leo mara baada ya kufungua kituo cha Afya
cha Nanyala kilichopo kata ya Nanyala wilayani Mbozi kitakachotoa huduma
kwa wakazi zaidi ya elfu kumi ikiwa siku ya pili ya ziara yake ya siku 5
katika mkoa wa Songwe. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...