Hiari yashinda utumwa. Hayo ni maneno yaliyosemwa na Wana-Same baada ya kupokea taarifa inayoonyesha athari za magonjwa yasiyoambukiza ambayo mengi yanatokana na kutofanya mazoezi na kutokula vyakula sahihi. 
Mratibu wa michezo ameagizwa kupanga ratiba ya wananchi  kufanya mazoezi kila wiki baada ya wananchi hao kuagizwa kufanya mazoezi ya japo nusu saa kila siku ili vijana waonesha mwamko kuliko watu wazima. 
Mkuu wa Wilaya ya Same Mhe. Rosemary Sitaki ameelekeza elimu itolewe nusu saa kila baada ya mazoezi ili kuongeza mvuto wa watu kuja kwenye mazoezi. 
Mada zenye nguvu kujadiliwa ikiwa ni pamoja na kusikiliza kero kutoka kwa wananchi mbalimbali. 
Hakika " Same is not the same"
Mazoezi yaliyoongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Same Mhe. Rosemary Sitaki
Mkuu wa Wilaya ya Same Mhe. Rosemary Sitaki akitoa nasaha za umuhimu wa mazoezi ya kila siku
Mkuu wa Wilaya ya Same Mhe. Rosemary Sitaki akiwa na vijana waliodamka kufanya mazoezi Jumamosi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...