TatuMzuka, mchezo wa namba unaoongoza nchini Tanzania leo umemkabidhi Mshindi wa kampeini ya ‘SupaMzuka Cup’ aliyeshinda katika fainali tarehe 15 Julai 2018 kitita cha milioni 300 za kitanzania.

Abeid Amri, 28 anayeishi Mbagala Wilaya ya Temeke Dar es Salaam ndiye ameibuka mshindi wa Jackpot kubwa kuwahi kutokea nchini Tanzania. Amri hakushinda peke yake bali alichagua timu yake ya watu 10 ili kukamilisha timu yake ya watu 11 ambapo kila mmoja amepata milioni 1.

“Tumepata faraja kubwa kushuhudia Mtanzania mwenzetu akipata ushindi mkubwa kiasi hiki. Umetuandikia historia leo kwa sababu haijawahi kutokea nchini Tanzania mtu kushinda million 300. ” Alisema Bwana Sebastian Maganga, Mkurugenzi wa mawasiliano wa TatuMzuka

Kwa Msimu huu wa SupaMzuka Jackpot watu wamecheza na kushinda na marafiki, na Bwana Amri pia alichagua timu yake ambao ni; 1 Mwanaidi Omary, 2.Subira Issa 3. Jasmin Issa 4. Shufwaa Issa 5. Farhat Issa 6. Omary Issa, 7. Amin Issa 8. Mwanaasha Omary, 9. Agness Samwel, 10. Magdalena.

“Mimi sijala vizuri, wala kulala tangu siku hiyo jumapili. Kila saa nawaza kama ni ndoto alafu nitaamka, lakini sasa naamini kabisa kwamba ni kweli nimeshinda” aliezea Amri. “Nina furaha sana na pia kushinda na marafiki, najiskia kama wengi tumeshinda!” alisisitiza Amri.

Mkurugenzi wa mawasiliano wa TatuMzuka Sebastian Maganga akizungumza mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo pichani),wakati wa akimtambulisha Mshindi wa kampeini ya ‘SupaMzuka Cup’ aliyeshinda katika fainali tarehe 15 Julai 2018 kitita cha milioni 300 za kitanzania,Abeid Amri mkazi kutoka Mbagala

Abeid Amri, 28 anayeishi Mbagala Wilaya ya Temeke Dar es Salaam ndiye ameibuka mshindi wa Jackpot kubwa kuwahi kutokea nchini Tanzania. Amri hakushinda peke yake bali alichagua timu yake ya watu 10 ili kukamilisha timu yake ya watu 11 ambapo kila mmoja amepata milioni 1. Mwakilishi kutoka kampuni ya michezo ya kubahatisha Abdallah Hemed
Wanahabari wakifuatilia tukio hilo 
Mkurugenzi wa mawasiliano wa TatuMzuka Sebastian Maganga akimkabidhi mfano wa hundi Mshindi wa kampeini ya ‘SupaMzuka Cup’ aliyeshinda katika fainali tarehe 15 Julai 2018 kitita cha milioni 300 za kitanzania,Abeid Amri mkazi kutoka Mbagala

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...