Mbunge wa Songea Mjini, Dk. Damas Ndumbaro akimkabidhi zawadi ya nishani ya baiskeli mshindi wa kwanza katika mbio za baiskeli 100KM za Tamasha la Majimaji Selebuka, Masunda Duba wa Simiyu. Pia alitwaa zawadi ikiwamo ya washindi watatu wa kwanza kupata fursa ya kutafutiwa mashindano nje ya nchi na kugharimiwa kila kitu na Taasisi ya SOMI.
Bingwa wa mbio za baiskeli 100KM za tamasha la kila mwaka la Majimaji Selebuka, Masunda Duba akishangalia baada ya kuhitimisha mbio hizo ambazo zilikuwa ni kutoka Wilaya ya Mbinga hadi Manispaa ya Songea.
. Bingwa wa mbio za baiskeli 100KM, Masunda Duba, akichuana vikali na Boniphace Masuda aliyeshika nafasi ya pili katika shindano lililoratibiwa na Taasisi ya SOMI kupitia Tamasha la Majimaji Selebuka.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...