Katibu Tawala wilaya ya Temeke Ndugu Hashimu Komba (kwa niaba ya MKuu wa Wilaya),akimkabidhi Kombe la Tatu Mzuka kwa kijana mkazi wa Mbagala,Abeid Amir aliyejinyakulia kitita cha shilingi Milioni 300,alipokwenda kutambulishwa kwa Mkuu wa Wilaya ya Temeke.Katika mazungumzo yake na Uongozi wa Wilaya mshindi huyo ameahidi kuchangia kiasi cha shilingi milioni mbili kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa kituo cha Polisi kinachojengwa Mbagala.
 Mshindi wa Milioni 300 za Supa Mzuka Cup 2018 Abeid Amir akipokelewa kwa shangwe,nderemo na vifijo  mara baada ya kuwasili nyumbani kwao Mbagala-Kilungule,ambapo pia alipokelewa vyema na viongozi wa serikali ya Mtaa kwa heshima kubwa.
  Mshindi wa Milioni 300 za Supa Mzuka Cup 2018 Abeid Amir akipokelewa kwa shangwe na Diwani wa Kata ya Kilungule Said Fella na akiwa sambamba na Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa wa Kata ya Zomboko Ndugu Hemed Said Njiwa,mara alipowasili nyumbani kwao Mbagala-Kilungule
Diwani wa Kata ya Kilungule Said Fella akizungumza machache mbele ya wageni waalikwa mbalimbali waliofika kumpokea mshindi huyo wa Milioni 300 za Supa Mzuka Cup 2018.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...