Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Mh. Benjamini Mkapa alipowasili nyumbani kwake Msasani, jijini Dar es salaam leo kuhani msiba wa Baba Mzazi wa Mama Salma Kikwete, Marehemu Mzee Rashid Mkwachu.
 Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Mh. Benjamini Mkapa akisalimiana na Mke wa Mh. Jakaya Kikwete, Mama Salma Kikwete wakati alipofika kuhani Msiba wa Baba yake, Marehemu Mzee Rashid Mkwachu uliotokea hivi karibuni. Mh. Mkapa aliambatana na Mkewe Mama Anna Mkapa. Kulia ni Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete.
 Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwaeleza jambo Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Mh. Benjamini Mkapa na Mkewe Mama Anna Mkapa, wakati walipofika nyumbani kwake, Msasani jijini Dar es salaam leo kuhani msiba wa Baba Mzazi wa Mama Salma Kikwete, Marehemu Mzee Rashid Mkwachu.
 Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Makamu Wa Rais Mstaafu, Dkt. Mohamed Gharib Bilal alipowasili nyumbani kwake Msasani, jijini Dar es salaam leo kuhani msiba wa Baba Mzazi wa Mama Salma Kikwete, Marehemu Mzee Rashid Mkwachu.
 Makamu Wa Rais Mstaafu, Dkt. Mohamed Gharib Bilal akimpa pole Mama Salma Kikwete, kwa kufiwa na Baba yake Marehemu Mzee Rashid Mkwachu. Dkt. Bilal aliambatana na Wake zake, Mama Zakhia na Mama Asha Bilal.
 Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimueleza jambo Makamu wa Rais Mstaafu Dkt. Mohamed Gharib Bilal na Wake zake, Mama Zakhia na Mama Asha Bilal, walipofika nyumbani kwake, Msasani jijini Dar es salaam leo kuhani msiba wa Baba Mzazi wa Mama Salma Kikwete, Marehemu Mzee Rashid Mkwachu.
 Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mh. Kangi Lugola akitoa pole ya msiba kwa Mama Salma Kikwete, aliyefiwa na Baba yake Marehemu Mzee Rashid Mkwachu. 

Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akimkaribisha nyumbani kwake, Jaji Mkuu Mstaafu, Augustino Ramadhan wakati alipofika kuhani msiba wa  Baba Mzazi wa Mama Salma Kikwete, Marehemu Mzee Rashid Mkwachu.
 Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (wa pili kushoto) akimkabidhi Mke wa Rais Mstaafu, Mama Salma Kikwete Rambirambi iliyotolewa na Wabunge kufuatia kufiwa na Baba yake, Marehemu Mzee Rashid Mkwachu. kushoto ni Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akishuhudia. Naibu Waziri Mgalu aliambatana na Mh. Hawa Ghasia.

BOFYA HAPA KUONA PICHA ZAIDI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...