Padri wa Kanisa la Anglikana, Jaji Mkuu Mstaafu Augustino Ramadhan akiongoza ibada ya kumbukumbu ya marehemu Elizabeth Shaba mke wa Profesa James Shaba aliye patwa na mauti Julai Mosi mwaka huu na kuzikwa Julai 7, Chicago, Marekani. Ibada hiyo imefanyika leo kwenye Kanisa la St Albano Angilkana, jijini Dar es Salaam.
Marehemu ambaye alikuwa anaishi na mumewe nchini Marekani mpaka anakutwa na mauti alikuwa Muuguzi Mshauri wa Ubalozi wa Kanada. Alioana na Profesa Shaba mwaka 1963. PICHA NA RICHARD MWAIKENDA
Baadhi ya ndugu, jamaa na marafiki wakishiriki kwenye Ibada hiyo
Anna Nyerere ambaye ni mtoto wa Baba wa Taifa, Hayati Julius Nyerere, akishiriki katika Ibada hiyo
James (KANGWAFA) pole sana. Nakuombea kila la kheri
ReplyDeleteIbrahim A Manthy