Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga limeendesha mafunzo kuhusu masuala ya usalama barabarani kwa wamiliki na madereva wa magari,pikipiki na bajaji ikiwa ni sehemu ya njia za kukabiliana na ajali zinazojitokeza na kusababisha vifo na majeruhi. 

Mafunzo hayo yaliyofunguliwa na Mkuu wa wilaya ya Shinyanga,Josephine Matiro yamefanyika leo Alhamis Julai 12,2018 katika ukumbi wa Bwalo la Polisi mjini Shinyanga. 

Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo hayo,Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro alisema suala la utii wa sheria za barabarani ni jukumu la watu wote hivyo kila mmoja lazima azingatie sheria za barabarani ili kuepuka ajali zisizo za lazima.

"Madereva ni wadau wakuu wa kuzuia ajali za barabarani, nalipongeza jeshi la polisi kwa kuona umuhimu na wadau hawa ili kuwapa elimu hii kwani madereva wakisikiliza na kufanyia kazi elimu hii hakika ajali hazitatokea mkoani Shinyanga",alieleza Matiro.

"Ili kutokomeza ajali,ni vyema jeshi la polisi likaendelea kufanya doria katika barabara kuu, kukagua leseni na kuhakikisha magari yote mabovu hayaiingii barabarani lakini pia kutoa elimu kwa wadau wote wakiwemo wanafunzi",aliongeza Matiro.
Kulia ni Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Shinyanga,ACP Simon Haule akimuonesha Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro ratiba ya mada zinazofundishwa kwa wamiliki na waendeshaji wa vyombo vya moto ikiwemo magari,pikipiki na bajaji.
Kushoto ni Mkuu wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia Mkoa wa Shinyanga SSP Richard George Abwaoakiteta jambo na Mkuu wa Kikosi cha Usalama Barabarani mkoa wa Shinyanga ASP Anthony Gwandu.
Dereva na mmiliki wa Tax na pikipiki, Omari Gindu akiomba askari wa usalama barabarani 'Trafiki' nao wapewe elimu ya usalama barabarani akidai baadhi yao hawajui sheria hivyo kukamata ovyo madereva na kuchangia kutokea kwa ajali
Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoa wa Shinyanga,ACP Simon Haule akisisitiza kuwa jeshi la polisi litaendelea kuwachukulia hatua za kisheria madereva watakaokiuka sheria za usalama barabarani.Kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro . Kulia ni Mkuu wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia Mkoa wa Shinyanga SSP Richard George Abwao
Madereva na wamiliki wa vyombo vya moto wakiapa kuzingatia sheria za barabarani ili kutokomeza ajali mkoani Shinyanga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...