*Ahimiza hivyo kujikita kujenga uchumi imara ili wananchi wapate huduma bora.
Na Chalila Kibuda,Globu ya jamii
UKOMBOZI wa sasa kwa vyama tawala katika nchi za Afrika ni vema wakajikita katika katika kujenga uchumi katika sekta mbalimbali ili wananchi wapate huduma bora.
Hayo ameyasema Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dk.John Magufuli wakati akifungua Mkutano wa Vyama vya siasa ambavyo vilivyopigania ukombozi kwa nchi za Kusini mwa Afrika ambapo vina uhusiano na Chama cha Kikomonisti cha China (CPC) uliofanyika leo katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Rais Dk.John Pombe Magufuli amesema kuwa chama cha CPC kimekuwa na uhusiano ya muda mrefu na kilisaidia ukombozi katika Afrika kwa kutoa silaha lakini sasa wamekuwa na maendeleo ambapo lazima kujifunza kutoka kwao.
Amesema kuwa nchi za Afrika zitoke katika mnyororo wa unyonyaji na kuingia katika uchumi wa kujitegemea. Amesema kuwa nchi ya China imekuwa ikitoa msaada bila masharti na kwamba kinachofanyika maelewano na msaada unatoka.
Rais wa Jamhuri ya Muungano ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia viongozi wa vyama vya Siasa kutoka nchi za mbalimbali za Afrika kabla ya kufungua mkutano kati ya viongozi wa vyama hivyo na Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) katika ukumbi wa Serena Hotel jijini Dar es Salaam.
Na Chalila Kibuda,Globu ya jamii
UKOMBOZI wa sasa kwa vyama tawala katika nchi za Afrika ni vema wakajikita katika katika kujenga uchumi katika sekta mbalimbali ili wananchi wapate huduma bora.
Hayo ameyasema Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Rais Dk.John Magufuli wakati akifungua Mkutano wa Vyama vya siasa ambavyo vilivyopigania ukombozi kwa nchi za Kusini mwa Afrika ambapo vina uhusiano na Chama cha Kikomonisti cha China (CPC) uliofanyika leo katika hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Rais Dk.John Pombe Magufuli amesema kuwa chama cha CPC kimekuwa na uhusiano ya muda mrefu na kilisaidia ukombozi katika Afrika kwa kutoa silaha lakini sasa wamekuwa na maendeleo ambapo lazima kujifunza kutoka kwao.
Amesema kuwa nchi za Afrika zitoke katika mnyororo wa unyonyaji na kuingia katika uchumi wa kujitegemea. Amesema kuwa nchi ya China imekuwa ikitoa msaada bila masharti na kwamba kinachofanyika maelewano na msaada unatoka.
Rais wa Jamhuri ya Muungano ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia viongozi wa vyama vya Siasa kutoka nchi za mbalimbali za Afrika kabla ya kufungua mkutano kati ya viongozi wa vyama hivyo na Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) katika ukumbi wa Serena Hotel jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Idara ya Mahusiano ya kimataifa na Waziri wa Mahusiano wa Kimataifa wa Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) Song Tao akizungumza katika mkutano huo wa viongozi wa vyama vya Siasa kutoka nchi za mbalimbali za Afrika na Chama hicho cha CPC jijini Dar es Salaam.
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Bashiru Ally akihutubia katika mkutano huo.
Washiriki wa Mkutano huo wakifatilia kwa makini hotuba mbalimbali zilizokuwa zikitolewa ukumbini hapo katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. John Pombe Magufuli akiagana na Mkuu wa Idara ya Mahusiano ya kimataifa na Waziri wa Mahusiano wa Kimataifa wa Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) Song Tao mara baada ya kufungua mkutano huo jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...