Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
SERIKALI imesema haitavivumilia vyuo ambavyo vitabainika vinatoa mafunzo yake kinyume na utaratibu uliowekwa na lengo ni kuhakikisha vijana wanapata elimu bora.
Pia imeiagiza Tume ya Vyuo Vikuu Nchini (TCU), kuongeza kasi ya ukaguzi na kuvifungia vyuo hivyo bila kujali ni vya umma au binafsi na kufafanuliwa Serikali hutenga Sh.bilioni 427.5 kwa ajili ya utoaji wa elimu kwa vyuo vya elimu ya juu nchini, hivyo haitarajii kuona madudu yanafanyika.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako wakati anafungua maonesho ya 13 ya Vyuo vya Elimu ya Juu katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam.
Amesema Serikali haitaweza kuvumilia uwepo wa vyuo visivyokuwa na sifa nchini kwani vimekuwa ni chanzo vya kuzalisha uwepo wa wanafunzi wasio na sifa.
Prof.Joyce amesema hivi karibuni Serikali ilifanya ukaguzi kwa baadhi ya vyuo na kubaini kuwepo kwa programu nyingi zilizokuwa zikiendeshwa kinyume cha taratibu.
“Sasa TCU ongezeni kasi ya ukaguzi kwa vyuo vyote nchini na endapo mkibaini viko baadhi vinaendesha mafunzo kinyume cha taratibu zilizoweka aidha kiwe cha Umma au binafsi fungia mara moja.
Waziri wa Elimu wa Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akizungumza katika Maonesho ya Vyuo vikuu nchini pamoja na vya nje vinavyoshiriki maonesho hayo katika viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar Salaam.
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako akipata maelezo kutoka kwa Afisa Habari Mwandamizi wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu Venaranda Malima kuhusiana Bodi hiyo katika maonesho ya vyuo Vikuu.
Wanafuzi wakipata maelezo kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Uhusiano wa Umma wa Taasisi ya Uhasibu Nchini (TIA) Lilian Rugaitika. Kuhusiana na kozi wanazozitoa katika maonesho ya vyuo vikuu jijini Dar es Salaam.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...