Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii
ROBO fainali ya Michuano ya Sprite BBall Kings imefanyika mwishoni mwa wiki hii na timu nne kufanikiwa kuvuka kwenda hatua inayofuata ya nusu fainali.

Mechi hizo zilizochezwa ndani wa Uwanja wa Ndani wa Taifa zilikuwa za ushindani mkubwa sana huku Bingwa mtetezi Mchenga BBall Stars akifanikiwa kushinda na kusonga hatua inayofuata.

Katoka mchezo wa kwanza uliokwakutanisha Water Institute dhidi ya Flying Dribblers uliweza kumalizika kwa Flyinh Dribllers kuibuka na  ushindi wa vikapu 100 dhidi ya 64

Mchezo wa pili uliwakutanisha Team Kiza akichuana na DMI, na katika mchezo huo DMI walikubali kichapo cha vikapu 82 kwa 47 vya DIM.

Mchenga Bball Stars alichuana na St Joseph katika mchezo wa tatu, mechi iliyokuwa na ushindani mkubwa na mpaka filimbi ya mwisho inapulizwa Mchenga akafanikiwa kuvuka kwa vikapu 84 dhidi ya vikapu 67 vya St Joseph.

Mechi ya mwisho ilikua ni Temeke Heroes dhidi ya Portland iliyohitimisha idadi ya timu nne za kuingia nusu fainali, na Portland wakihitimisha mechi hiyo kwa kuibuka mshindi kwa vikapu 83 dhidi ya vikapu 70 vya Temeke Heroes.
 Nahodha wa Timu ya Mchenga BBall Stars Mohamed Yusuph akijaribu kuwatoka wachezaji wa St Joseph wakati wa mechi ya robo fainali ya Michuano ya Sprite BBall Kings uliomalizika kwa Mchenga kuibuka na ushindi wa Vikapu 84 kwa 47 vya St Joseph.

 Vuta nikuvute wakati wa mechi ya robo fainali ya Michuano ya Sprite BBall Kings uliomalizika kwa Mchenga kuibuka na ushindi wa Vikapu 84 kwa 47 vya St Joseph.
Mashabiki waliojitokeza kuangalia michuano ya Sprite BBall Kings katika Uwanja wa Ndani wa Taifa.
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Kikapu (TBF) Phares Magessa (kulia) akiwa pamoja na Katibu Mkuu wa TBF Mike Mwita wakishuhudia robo fainali ya Michuano ya Sprite BBall Kings.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...