Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.
JUMUIYA ya Umoja  wa Wanawake  Tanzania (UWT) Wilaya ya Temeke wamempongeza Mwenyekiti wa Chama hicho na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufulu kwa kuweza kutekeleza ahadi ya kununua ndege ya nne kati ya saba alizoziahidi.

UWT Temeke wamesema kuwa hiyo ni moja ya ahadi zilizoanishwa katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi na wamemuomba aweze kutimiza ahadi zote ili kuhakikisha upinzani wanakosa la kusema.

Akizungumza na wajumbe wa UWT Wilaya ya Temeke, Mgeni rasmi Mbunge wa Viti Maalum  Mkoa wa Dar es Salaam Mariam Kisangi  amesema kuwa serikali ya awamu ya tano ya Chama cha Mapinduzi imedhamiria kutimiza ahadi zote zilizoanishwa wakati wa kampeni  na tayari zinafanyiwa kazi ikiwemo kununua ndege ya nne kati ya saba na zile zitakazoanza kutekelezwa kwenye bajeti ya 2018/19.

"Rais wetu Dkt Magufuli aliahidi kununua ndege saba zitakazokuwa mali yetu na mpaka sasa ameshanunua ndege  ikiwemo Boeing  787-8 Dreamliner  na kutimiza idadi ya ndege nne kati ya saba alizotoa ahadi kwenye kampeni zake mwaka 2015,"amesema Mb Mariam.
Mbunge wa Viti Maalum  Mkoa wa Dar es Salaam Mariam Kisangi  akizungumza na wajumbe wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Wilaya ya Temeke wakati wa hafka yao ya kumpongeza Mwenyekiti wa Chama na Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa kununua ndege ya nne Boeing 787-7 Dreamliner kati ya saba alizozitoa katika ahadi yake wakati wa kampeni za uchaguzi 2015.
 Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake (UWT) Wilaya ya Temeke, Rukia Kamal akizungumza na wajumbe wa UWT Temeke wakati wa hafla ya kumpongeza  Mwenyekiti wa Chama na Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa kununua ndege ya nne Boeing 787-7 Dreamliner kati ya saba alizozitoa katika ahadi yake wakati wa kampeni za uchaguzi 2015.

Katibu wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake (UWT) Wilaya ya Temeke Kimenta Mavala akielezea jambo mbele ya wajumbe na Mgeni rasmi wa hafla yakumpongeza Mwenyekiti wa Chama na Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa kununua ndege ya nne Boeing 787-7 Dreamliner kati ya saba alizozitoa katika ahadi yake wakati wa kampeni za uchaguzi 2015.
 Wajumbe wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake (UWT)  Wilaya ya Temeke wakiwa katika hafla ya kumpongeza Mwenyekiti wa Chama na Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa kununua ndege ya nne Boeing 787-7 Dreamliner kati ya saba alizozitoa katika ahadi yake wakati wa kampeni za uchaguzi 2015.
 Mbunge wa Viti Maalum  Mkoa wa Dar es Salaam Mariam Kisangi akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wajumbe  wa UWT Wilaya ya Temeke wakati wa hafla ya kumpongeza  Mwenyekiti wa Chama na Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli kwa kununua ndege ya nne Boeing 787-7 Dreamliner kati ya saba alizozitoa katika ahadi yake wakati wa kampeni za uchaguzi 2015.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...