Na Dixon Busagaga,Moshi

VIONGOZI watano wa Chama cha Ushirika mkoa wa Kilimanjaro(KNCU LTD) na Kiwanda cha Kukoboa Kahawa cha Tanganyika (TCCCO) leo wamepandishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi ,Moshi na kusomewa Mashtaka tofauti yakiwemo ya uhujumu Uchumi.

Waliofikishwa Mahakamani na kupandishwa Kizimbani ni pamoja na Mwenyekiti Mstaafu wa Chama Kikuu cha Ushirika ,Kilimanjaro (KNCU) Aloisi Kitau (70) Makamu Mwenyekiti mstaafu wa KNCU,Hatibu Mwanga(70) na Meneeja Mkuu wa KNCU ,Honest Temba (38).

Wengine waliofikishwa mahamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi ,Pamela Mazengo ni aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Kampuni ya Kukoboa Kahawa (TCCC0) Maynard Swai (57) na aliyekuwa Meneja Mkuu wa TCCCo ,Andrew Kleruu wanaotajwa kukiuka sheria wakati wa ununuzi wa mtambo wa kukoboa Kahawa.

Wakili wa serikali Jaqueline Nyantori aliieleza mahakamani kuwa Washitakiwa ,Maynard Swai na Andrew Kleruu wanakabiliwa na makosa mawili huku akiyataja kuwa ni Matumizi mabaya ya ofisi na kusababishia serikali hasara .

Upande wa Jamhuri katika Shauri hilo unawakilishwa na Wakili wa serikali Mandamizi ,Shadrack Martin,Wakili wa serikali Mwandamizi ,Abdalah Chavula na Wakili wa serijali Jacqueline Nyantori huku Wakili Julius Semali akimtetea Mshtakiwa Honest Temba na Wakili Captain Sawayaeli Shoo akimtetea Mshtakiwa Hatibu Mwanga.



Watuhumiwa hao wakishushwa Mahakamani mapema leo chini ya Ulinzi wa Jeshi la Polisi,kusomewa mashtaka yao

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...