Na Mwandishi wetu
WABUNGE wa mkoa wa Kigoma walipata nafasi ya kutaarifiwa mradi wa pamoja mkoa wa Kigoma na Umoja wa Mataifa ambao umejikita katika kutekeleza Mpango wa Taifa wa Maendeleo na pia kutekeleza shughuli mbali mbali zinazolenga kufikia malengo endelevu ya dunia.
Akifungua mkutano huo Mkuu wa mkoa wa Kigoma, Brigedia Jenerali mstaafu Emmanuel Maganga aliwataka washiriki wa mkutano huo kufuatilia kwa makini hatua iliyofikiwa ya mradi huo na kutoa mapendekezo yao.
Baadhi ya shughuli za mradi huo zimeanza kutekelezwa hususan katika maeneo ya Kilimo, uwezeshaji wa wanawake na vijana kiuchumi, kutokomeza vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia kwa watoto na kina mama pamoja na elimu.
Mkuu huyo wa mkoa aliwataka waheshimiwa wabunge kutumia fursa waliyoipata kupokea taarifa kuhusu mradi na kutoa ushauri wa namna ya kufanikisha malengo yaliyowekwa ili kuwaletea maendeleo kwa wananchi wa mkoa wa Kigoma.
“Mkoa wa Kigoma ni Mkubwa na tunatamani kuona mradi huu unapanuka kujumuisha wilaya zote na pia sekta nyingine muhimu kama afya. “ alisema Maganga ambaye alisema kama serikali wako tayari kushirikiana na wadau wote wenye mapenzi na mkoa wa Kigoma wataliona hilo.
Katika mkutano huo ambao pia umehudhuriwa na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini Tanzania, Alvaro Rodriguez na wadau  wengine wa maendeleo, misingi imara ya ushirikiano kwa ufanikishaji wa maendeleo ya mkoa wa Kigoma kwa ujumla yalizungumzwa na kuafikiwa.  

 Mkuu wa mkoa wa Kigoma, Brigedia Jenerali mstaafu Emmanuel Maganga (kulia) akifungua mkutano ulioandaliwa kwa Wabunge wa mkoa wa Kigoma juu ya mradi wa pamoja na Umoja wa Mataifa uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za Umoja wa Mataifa jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez na kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma, Charles Pallangyo.
 Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akitoa neno la ukaribisho kutoka Umoja wa Mataifa wakati wa mkutano ulioandaliwa kwa Wabunge wa mkoa wa Kigoma juu ya mradi wa pamoja mkoa wa Kigoma na Umoja wa Mataifa (UN-KJP) uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za Umoja wa Mataifa jijini Dar es Salaam. Katikati ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Kigoma, Charles Pallangyo na kushoto ni Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa Kigoma, Evance Siangicha.
 Mwenyekiti wa Wabunge wa mkoa wa Kigoma ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kasulu Mjini-CCM,  Daniel Nsanzugwanko akitoa salamu kwa niaba ya Wabunge wa mkoa wa Kigoma wakati mkutano ulioandaliwa kwa Wabunge hao juu ya mradi wa pamoja na Umoja wa Mataifa uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za Umoja wa Mataifa jijini Dar es Salaam.
 Mwakilishi wa Umoja wa Mataifa Kigoma, Evance Siangicha (kulia) akiwasilisha muhtasari wa mradi wa pamoja wa Umoja wa Mataifa kwa Wabunge wa mkoa wa Kigoma wakati wa mkutano maalum ulioandaliwa juu ya mradi huo wa pamoja uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za Umoja wa Mataifa.
 Mbunge wa Kigoma Kaskazini kupitia tiketi ya ACT Wazalendo, Zitto Kabwe akifafanua jambo wakati wa majadiliano juu ya mradi wa pamoja wa Kigoma na Umoja wa Mataifa wakati wa mkutano maalum na Wabunge wa mkoa huo ulioandaliwa na UN na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za Umoja wa Mataifa.
 Kaimu Mkuu wa Ofisi za Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) nchini, Bi. Faith Shayo (kulia) akielezea kuhusu mradi wa UNESCO kwa kushirikiana na UN Women pamoja na UNFPA unaofadhiliwa na Shirika la Misaada la Korea (KOICA) katika eneo la elimu wakati wa mkutano juu ya mradi wa pamoja wa Kigoma na Umoja wa Mataifa wakati wa mkutano maalum na Wabunge wa mkoa huo ulioandaliwa na UN na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za Umoja wa Mataifa.
 Picha ya pamoja ya Waheshimiwa Wabunge wa mkoa wa Kigoma na Wafanyakazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa mara baada ya kumalizika kwa mkutano maalum juu ya mradi wa pamoja wa Kigoma na Umoja wa Mataifa na Wabunge hao ulioandaliwa na UN na kufanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za Umoja wa Mataifa.


KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...