Wakati tukielekea kwenye uchaguzi mdogo wa Jimbo la Buyungu na kata 77 utakaofanyika tarehe 12 Agosti, 2018, nachukue fursa hii kuwakumbusha wadau wote hususani vyama vya siasa, wagombea na Asasi za kiraia kuzingatia matakwa ya Sheria ya Gharama za Uchaguzi na Sheria ya Vyama vya Siasa.

Sheria ya Gharama za uchaguzi inamtaka kila Mgombea wa Ubunge na Udiwani kuweka wazi mapato na matumizi ya gharama anazotarajia kuzitumia wakati wa uchaguzi husika kwa kujaza fomu maalumu ( EE1 & EE2) ambazo hujazwa na kuwasilishwa kwenye mamlaka husika ndani ya siku saba, kuanzia siku ya uteuzi wa wagombea. Hivyo ninasisitiza ujazaji sahihi wa fomu hizo maalumu ili kukidhi matakwa ya Sheria.

Pia, ninawakumbusha wagombea, vyama vya siasa na umma kwa ujumla kuepuka kufanya vitendo vinavyokatazwa na Sheria za nchi hususani Kanuni za Maadili ya Vyama vya Siasa, Sheria ya Vyama vya Siasa na Sheria ya Gharama za Uchaguzi ili kuhakikisha kuwa uchaguzi unakuwa huru na wa haki na pia unaendeshwa katika hali ya Amani na utulivu.
Nichukue nafasi hii pia kuwatakia Wadau wote maandalizi na uchaguzi Mwema.

Jaji Francis S.K. Mutungi
MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...